WATU SITA WAUAWA KWENYE GHASIA SOMALIA
 
Wapiganaji wa Al-shabaab
 
 
Takriban watu sita wameuawa katika ghasia katikati mwa 
Somali.
Ijumaa usiku, wanamgambo kutoka kundi la Alshabaab walishambulia kambi moja 
ya wanajeshi wa Umoja wa Afrika katika mji wa Buloburde, yapata kilomita 200 
kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.
Vikosi vya Amisom viliuteka mji wa Buloburde kutoka kwa Alshabaab mapema 
mwaka huu, lakini wanamgambo hao bado wanadhibiti eneo kubwa la viunga mwa mji 
huo.
Wameendelea kutekeleza mashambulizi mjini Mogadishu ili kujaribu kuiondoa 
serikali inayoungwa mkono na jamii ya kimataifa.(TK)
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni