Elizabeth Michael, maarufu kama Lulu
Mahakama kuu ya Dar es salaam imemhukumu muigizaji
wa filamu, Elizabeth Michael, maarufu kama 'Lulu', kifungo cha miaka
miwili baada ya kumtia hatiani kwa kuua bila kukusudia msanii mwenzake
marehemu Steven Kanumba.Marehemu Steven Kanumba alifariki majira ya saa nane usiku,mnamo mwaka 2012 baada ya kutokea mzozo kati yake na Elizabeth Michael ambaye inaaminika kuwa walikuwa na uhusiano wa Kimapenzi.

Marehemu ambaye alizaliwa mwaka 1984, alianza kujipatia umaarufu mwanzoni mwa mwaka 2000 wakati huo akiigiza katika michezo ya runinga kupitia kundi la maigizo la Kaole Sanaa.

Mazishi yake yalichukua sura ya kitaifa kutokana na umaarufu aliojijengea msanii huyo katika jamii ya watanzania na hata nchi za nje.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni