Jumatatu, 4 Mei 2015

FLOYD MAYWEATHER ANAMTAKA KHAN BAADA YA MANNY PACQUIAO

maypac
Baada ya pambano la karne kufanyika na matokeo kuwa mazuri kwa Floyd Mayweather swali aliloulizwa baada ya pambano ni kwamba atakuwa na pambano lingine akasema "yes, mwezi wa tisa ana pambano". Baada ya hapo alivyokuwa kwenye press conference alivyoulizwa nani utamtaka kwa ajili ya pambano lako la mwisho mwezi wa tisa. Mayweather alijibu kwa kifupi “Khan”.

Amir Khan ni bondia kutoka England ambaye na yeye ni bondia maarufu na mara nyingi amehusishwa kuhusu pambano kati yake na Mayweather. Pambano hilo ndio litakuwa la mwisho kwa Money Money. “Baada ya pambano langu la mwezi wa tisa nitastaafu kucheza tena boxing”.
amir

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni