Mwanamke mmoja nchini Italia amejioa yeye mwenyewe kwenye sherehe iliyokuwa na vazi kamili la harusi, keki na wageni 70.
"Ninaamini kuwa kila mmoja wetu ni lazima ajipende," alisema Luara Mesi mwenye miaka 40Wanaounga mkono ndoa kama hizo wanasema kuwa suala kuu ni kujipenda.
Laura anasema kuwa suala la kujioa lilimjia miaka miwili iliyopita, baada ya miaka 12 ya kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi.

"Ikiwa siku moja nitapata mwanamume ambaye nitapanga kuishi naye nitafurahi, lakini furaha yangu haimtegemei yeye."
Bi Mesi anasema kuwa yeye ndiye mwanamke wa Kwanza nchini Italia kufanya harusi ya mtu mmoja.

Hata hivyo Bi Mesi ametupilia mbali maoni hayo akisema hakuna mtu atakayezima tabasamu lake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni