Waziri
mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu ameelezea mshangao wake binafsi kwa
mwanajeshi wa Israeli wa asili ya Ethiopia ambaye alipigwa na polisi wa
Israeli hali iliyosababisha kutokea kwa maandamano.
Bwana Netanyahu alimuambia Damas Fikadeh kuwa kitendo hicho hakikubaliki, na madabiliko yanahitaji kufanywa.Wakati wa ghasi hizo za siku ya jumamosi usiku mjini Tel Aviv takriban watu 50 walijeruhiwa.
Akizungumza baada ya maandamano yenye ghasia mjini Tel Aviv bwana Rivlin alisema kuwa kidonda kilicho wazi kimeonekana nchini Israeli, lakini ghasia sio suluhu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni