 Ofisi ya Rais imesambaza mwongozo unaoweka masharti ambayo watumishi wa
 umma wanaotaka kusafiri nje ya nchi watatakiwa kutimiza ili wapewe 
kibali, ikiwa ni mkakati wa kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la 
kudhibiti safari holela za nje.
 Ofisi ya Rais imesambaza mwongozo unaoweka masharti ambayo watumishi wa
 umma wanaotaka kusafiri nje ya nchi watatakiwa kutimiza ili wapewe 
kibali, ikiwa ni mkakati wa kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la 
kudhibiti safari holela za nje.
Rais 
alitoa agizo hilo baada ya kikao baina yake na makatibu wa wizara 
kilichofanyika Ikulu siku chache baada ya kuapishwa, akisema ofisi yake 
ndiyo itakayotoa kibali kwa watumishi ambao wana safari za nje.
Kwa mujibu wa waraka huo, sharti la kwanza linalotakiwa kuzingatiwa na watumishi hao ni kuomba kibali kwa Katibu Mkuu Kiongozi.
Pili, kwa
 mujibu wa mwongozo huo, maombi yawasilishwe kwa msajili wa hazina kabla
 ya kwenda kwa Katibu Mkuu Kiongozi ili aweze kujenga hoja kwa kuzingatia umuhimu wake
 na tija itakayopatikana kutokana na safari hiyo.
Tatu, 
mtendaji mkuu wa shirika au taasisi apime maombi ya safari husika ili 
kuona kama yana tija na yana umuhimu wa kuombewa kibali kwa Katibu Mkuu Kongozi, kabla ya kuwasilishwa kwa msajili wa hazina, kwa mujibu wa 
mwongozo huo.
 
