Jumatatu, 30 Mei 2016
SHEKHE AUAWA KATIKA FUMANIZI
JESHI la Polisi Wilaya ya Tunduru, mkoani Ruvuma, linamshikilia mkazi wa Kijiji cha Likweso, Tarafa ya Mchoteka, Ally Mchumwa 
SAMATTA AIPELEKA GENK EUROPA LEAGUE
Tarehe May 29, Mbwana Samatta ameandika historia mpya kwenye maisha yake baada ya kuisaidia timu yake ya Genk kushinda mchezo wa fainali ya play off na hatimaye kufuzu kucheza michuano ya Ulaya (Europa League).
Samatta ambaye alianza kwenye kikosi cha kwanza cha Genk ameisaidia klabu yake kupata ushindi wa magoli 5-1 kwenye uwanja wao wa nyumbani (Cristal Arena) dhidi ya Sporting Charleroi.
Alhamisi, 19 Mei 2016
DOLA ZA KIMAREKANI BILIONI 3 KUTUMIKA KUANZISHA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA.
Waziri
 wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (kushoto) 
akiongea na Waandishi wa Habari (hawako pichani) kuhusu kuanza kwa mradi
 wa Mgodi wa kuchimba chuma na makaa ya mawe Liganga na Mchuchuma leo 
mjini Dodoma 19 Mei, 2016. Katikati ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge 
inayosimamia viwanda, biashara na uwekezaji, Mhe. Dkt. Dalaly Kafumu 
pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji toka Shirika la Maendeleo la Taifa 
(NDC), Bwana Mlingi Mkucha.
Mwenyekiti
 wa Kamati ya Bunge inayosimamia viwanda, biashara na uwekezaji, Mhe. 
Dkt. Dalaly Kafumu (kulia) akisisitiza jambo mbele ya Waandishi wa 
Habari (hawako pichani) kuhusu kuanza kwa mradi wa Mgodi wa kuchimba 
chuma na makaa ya mawe Liganga na Mchuchuma leo mjini Dodoma 19 Mei, 
2016. Kushoto ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles 
Mwijage.
Na Benedict Liwenga, MAELEZO, Dodoma.
JUMLA
 ya dola Bilioni 3 za Kimarekani zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa 
Mgodi wa Makaa ya Mawe na Chuma wa Liganga na Mchuchuma.Kauli hiyo 
imetolewa Leo mini Dodoma na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, 
Mhe. Charles Mwijage wakati akiongea na Waandishi wa habari mini Dodoma.
Jumatatu, 16 Mei 2016
Lidege likubwa zaidi duniani latua Australia
Maelfu ya watu 
nchini Australia wanaopenda ndege walikusanyika kutizama ndege kubwa 
zaidi duniani ya Antonov An-225 Mriya, ilipowasili mjini Perth nchini 
humo.
Ndege hiyo yenye urefu wa mita 84 na uzito wa tani 175 bila 
ya kubeba mzigo wala mafuta, ilikuwa ikisafirisha jenereta yenye uzito 
wa tani 117.KITISHO CHA BOMU CHAAHIRISHA MECHI YA MAN U
Hofu ya kuwepo bomu uwanjani imesababisha mechi ya Manchester United na Bournemouth kuahirishwa.
Mechi ya mwisho 
katika ligi ya soka ya uingereza, EPL, kati ya Manchester united na 
Bournemouth imeahairishwa kufuatia wasiwasi wa bomu, uwanjani Old 
Trafford.
Jisajili kwenye:
Maoni (Atom)
