Mshike mshike wa
kuwania ubingwa wa ligi kuu England umeendelea kushika kasi ambapo
Tottenham Hotspur walipata ushindi ugenini wa bao 1-0 dhidi ya Crystal
Palace.
Bao pekee la Spurs katika mchezo huo lilifungwa na kiungo
Christian Eriksen, katika dakika ya 78 ya mchezo na hivyo kuendelea
kuwakimbiza vinara wa ligi hiyo Chelsea, wanaongoza ligi kwa alama 78
huku Spurs wakiwa nafasi ya pili kwa alama 74.
Vibonde wa ligi Middlesbrough wakautumia vyema uwanja wa nyumbani wa Riverside kuwa kuwachapa kwa bao 1-0 vibonde wengine wa ligi Sunderland ambao ndio wanaburuza mkia katika ligi hiyo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni