Mbunge
 wa Mtama, Nape Nnauye ameuliza serikali imefikia wapi kutafuta soko la 
Mbaazi baada ya msimu uliopita matatizo ya soko kushusha bei kutoka Tshs 2,000 mpaka 150. Amesema serikali iliahidi Bungeni kuwa itahakikisha inahangaika kupata soko la kuaminika la zao hilo.
Nape
 amesema sasa ni msimu wa kilimo hicho, kama bado hali haieleweki 
wananchi washauriwe waachane na mbaazi na badala yake wajikite kwenye 
mazao mengine ambayo yana soko la uhakika.
Akijibu
 swali hilo naibu waziri wa kilimo, Eng. Stella Manyanya amemjibu kuwa 
ni kweli hakukuwa na hali inayoridhisha kwenye soko la mbaazi na ni 
kutokana na wadau waliokuwa wanategemewa sana ilikuwa ni India.


 

