UN YASEMA MAJESHI YA SUDAN KUSINI YALIBAKA NA KUUA
Jeshi la SPLA Linadaiwa kutekeleza mauaji hayo katika jimbo la Greater Upper Nile
Umoja
wa mataifa unasema kuwa Wajeshi wa Sudan Kusini wamewabaka kwa zamu
wasichana wengi kisha wakawachoma moto wakiwa majumbani mwao.
Kwa
mujibu wa ripoti hiyo mpya ya umoja wa mataifa ukatili huo ulitokea
katika eneo la Greater Upper Nile ambako kumekuwa na mapigano makali
kati ya vikosi vya serikali na waasi. UN:Jeshi la Sudan Kusini 'lilibaka na kuwachoma moto wasichana
Katika tukio moja, mwanamke
mmoja alilazimishwa kushika makaa ya moto huku akipigwa katika jaribio
la kumshinikiza kutambua waliko waasi. Kufikia sasa hakuna upande uliojibu madai hayo dhidi yao.
Umoja wa mataifa vile vile umelaumu pande zote hasimu kwa kuwalazimisha watoto kuwa wanajeshi, ubakaji na mauaji.
Kufikia sasa hakuna upande uliojibu madai hayo dhidi yao
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni