Mbunge wa
 Viti Maalumu kupitia chadema,Rose Kamili,akizungumza na waandishi wa 
habari jijini Dar es Salaam leo jioni kuhusiana na tuhuma alizozitoa 
mume wake kwamba waliishi kwa maisha ya kula mihogo na familia yake ili 
kuhakikisha Chadema inastawi na kuimarika jambo ambalo si la kweli 
walikuwa na maisha mazuri ya kawaida tu na kusema kuwa Dk.Slaa anapaswa 
awaombe radhi wataznzania kwa kufafanisha kula mihogo kuwa ni umaskini 
na kuongeza kwa kusema mbona ukienda katika mahoteli makubwa mihogo na 
viazi ipo na watu wenye pesa zao wanakula kama kawada.
 
akizungumzuia
 kuhusu matamshi aliyasema Dk.Slaa kwamba haongei na waziri mkuu 
mstaafu,Sumaye,mama rose kamili alisema kuwa wiki tatu zilizopita waziri
 mkuu huyo mstaafu aliomba namba za dk.slaa akampatia wakaongea vizuri 
bila shida yoyote ila anamshangaa juzi aliposema mbele ya waandishi wa 
habari kwamba hazungumzi na sumaye.
akizungumzia
 kuhusu kuja kwa Lowassa Chadema mama huyo alisema kuwa Dk.slaa 
alikuwepo katika kumkaribisha waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa 
kujiunga na chama hicho ni jambo la kushangaza akizungumza kwamba 
hakushiriki na pia wakati chokochoko hizo za kustaafu ukatibu wake 
alisema kuwa viongozi waandamizi wa chama cha mapinduzi walimfuata na 
kumshawishi kutoludi kwenye ukatibu mkuu wake huo atapewa ubunge wa 
kuteuliwa na rais atakayeapishwa na kupewa uwaziri katika serikali ya 
awamu ya tano.
Kamili 
alimaliza kwa kutoa rai kwa watanzania wote nchini kutomsikiliza 
Dk.Wilbrod Slaa na kuwasihi kuendelea kuwa na matumaini na mgombea wa 
urais wa Chadema,Edward Lowassa aliyesimamishwa na chama chao pamoja na 
umoja wa katiba ya wananchi (Ukawa) ili kukiondoa madarakani chama 
tawala.
 Linus Slaa.
Linus Slaa. 
 Emiliana Slaa.
Emiliana Slaa. 
 Mama Rose Kamili akizungumza kwa hisia kali.kushoto ni mtoto wake aliyezaa na Dk.Slaa aitwaye,Emiliana Slaa.
Mama Rose Kamili akizungumza kwa hisia kali.kushoto ni mtoto wake aliyezaa na Dk.Slaa aitwaye,Emiliana Slaa. 
 Mama Rose Kamili akizungumza kwa hisia kali.kulia ni mtoto wake, Linus Slaa.
Mama Rose Kamili akizungumza kwa hisia kali.kulia ni mtoto wake, Linus Slaa. 
 waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini leo
waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini leo 
Mbunge wa
 Viti Maalumu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Rose Kamili, 
akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana juu ya mume
 wake Dk.Wilbrod Slaa kuzungumza wakati akiwa Katibu mkuu wa chadema 
familia yake ilikula kwa shida kwa sababu ya kujenga chama hicho jambo 
ambalo si la kweli. Wengineo ni watoto wake, Linus Slaa (kulia) na 
Emiliana Slaa.
SOURCE:HABARI TANZANIA