Mkurugenzi
 Mkuu wa Kampuni ya The Dila Africa, Jumba Dickson, akizungumza na 
waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya ufugaji wa sungura unaweza 
ukawasaidia wakulima katika kujiongezea kipato kwa mbali na kuuza nyama 
yake lakini pia wana uwezo wa kuuza kinyesi, mkojo pamoja na ngozi 
yake,katika ziara ya mafunzo kuhusu mradi huo katika eneo la Kivungwi 
kata ya Vigwaza, Mkoa wa Pwani.
  Mkurugenzi
 Mkuu wa Kampuni ya The Dila Africa, Jumba Dickson,akiwaonesha waandishi
 moja ya sungura wanaopatikana katika shamba hilo, kulia ni Mjasiriamali
 na mfugaji wa sungura hao, Gladness Nyange, katika ziara ya mafunzo 
kuhusu mradi huo katika eneo la Kivungwi kata ya Vigwaza, Mkoa wa Pwani.
 Sehemu ya mabanda ya kufugia Sungura hao.
Mkurugenzi
 Mkuu wa Kampuni ya The Dila Africa, Jumba akifafanua jambo kwa Wandishi 
wa habari  katika ziara ya mafunzo  kuhusu mradi  huo  katika eneo la 
Kivungwi kata ya Vigwaza, Mkoa wa Pwani.
 Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii
WATANZANIA
 wameshauriwa kujihusisha na ufugaji wa sungura ili waweze kujiongezea 
kipato kutokana na mnyama huyo kuwa na faida nyingi.
Ushauri
 huo umetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya The Dila Africa, Jumba 
Dickson wakati akizungumza na waandishi wa habari waliokuwa katika ziara
 ya mafunzo kuhusu mradi huo jana katika eneo la Kivungwi kata ya 
Vigwaza, Mkoani Pwani.
Dickson
 alisema, ufugaji wa sungura unaweza utawanufaisha wakulima katika 
kujiongezea kipato  mbali na kuuza nyama yake wana uwezo wa kuuza 
kinyesi, mkojo pamoja na ngozi yake
“Tunawafundisha
 wakulima jinsi ya kufuga sungura ili waweze kunufaika, lakini wanaweza 
kujiuliza ni wapi wanaweza kuwauza wakishafikia hatua ya kuuzwa, sisi 
tunawapa soko kwa hiyo kikubwa kwa mkulima ni kufuga tu,” Dickson 
alisema.
Alisema
 kampuni yake ina mashamba ya sungura hivyo wanapoingia mkataba na 
wakulima wanaohitaji kufuga wanakubaliana mambo mbalimbali ikiwemo 
kuwatafutia masoko ambapo wao wenyewe wananunua sungura hao. 
Alisema
 mbali na faida ya kuuza nyama yake lakini pia wanaweza kuuza kinyesi, 
mkojo pamoja na ngozi yake.                                              
                                    
Naye
 Mjasiriamali na mfugaji wa sungura hao, Gladness Nyange alisema, kuna 
umuhimu wa kinamama  kutumia fursa ya ufugaji sungura ili kumudu 
kuwasomesha watoto wao badala ya kuwategemea waume zao.
Alisema
 licha ya kuwa sungura hao wanahitaji uangalizi wa hali ya juu katika 
kuwafuga lakini amekuwa akihakikisha kuwa wanaishi katika mazingira mazuri
 ili waweze kumpa faida.
“Huu
 ufugaji kwa kuwa ni mpya watu, wengi wanaweza kujiuliza inakuwaje au 
masoko watapata wapi...lakini mimi nilipoanza kufuga niliingia mkataba 
na hii kampuni na wao walinipa masoko ina maana kwa kila sungura wa kilo
 nne nauza kwa Sh 40,000,” Nyange alisema.
Nyange
 alishauri wajasiriamali na hasa wanawake kujiingiza katika ufugaji huo 
ili waweze kufanya mambo yao mbalimbali bila kuwategemea akinababa ambao
 wakati mwingine wanakuwa na majukumu memgi.
 







