Ripoti ya Umoja wa Mataifa inakadiria idadi ya watu 
India itaipiku ya China katika kipindi cha miaka saba ijayo na Nigeria 
inatarajiwa kuipiku Marekani na kuwa taifa la tatu duniani lenye idadi 
kubwa ya watu ifikapo 2050
Ripoti hiyo iliyotolewa na idara ya uchumi na masuala ya kijamii ya 
shirika la  kushughulikia idadi ya watu duniani katika Umoja wa Mataifa 
inakadiria kuwa idadi ya hivi sasa ya watu duniani ya takriban bilioni 
7.6 itaongezeka hadi watu bilioni 8.6 ifikapo mwaka 2030, bilioni 9.8 
ifikapo 2050 na bilioni 11.2 ifikapo mwaka 2100.
Inaripotiwa kuwa karibu watu miliioni 83 wanazaliwa duniani kila mwaka, dalili zinaoonyesha ongezeko litakaloendelea hata kama viwango vya uzazi vitashuka kama inavyoshuhudiwa tangu miaka ya 1960.
Inaripotiwa kuwa karibu watu miliioni 83 wanazaliwa duniani kila mwaka, dalili zinaoonyesha ongezeko litakaloendelea hata kama viwango vya uzazi vitashuka kama inavyoshuhudiwa tangu miaka ya 1960.
 


