Wamarekani wamchagua Trump kuwa rais wao
Wamarekani wamemchagua Donald Trump kuwa rais wa 45 wa nchi hiyo.
Amejipatia sauti 276 dhidi ya 218 za wawakilishi wa majimbo. Rais
mteule Trump amewahutubia wafuasi wa chama chake na wamarekani kwa
jumla. Mgombea wa chama cha Democrats Hillary Clinton amekubali kushindwa na ameshazungumza kwa simu na Donald Trump kumpongeza.
Jumatano, 9 Novemba 2016
MTOTO ASIPEWE JINA LA BABA PEKEE: ITALIA
Mahakama ya katiba
ya Italia imetoa hukumu dhidi ya sheria inayompatia moja kwa moja mtoto
anayezaliwa ndani ya ndoa jina la baba yake.
Mawakili walidai kuwa kuzuwia familia kuwapatia watoto wao majina ya babu zao wazaa mama ni ubaguzi dhidi ya wanawake.Jumanne, 8 Novemba 2016
WEZI WA KENYA KIBOKO: WAIBA MASHINE YA ATM NAIROBI
Picha ya Benki ya Equity, Kenya
Polisi nchini Kenya
katika jiji kuu Nairobi wamemkamata mlinzi wa Benki ya Equity kuhusiana
na wizi mwishoni mwa wiki ambapo wezi walitoweka na mtambo wa kutoa
pesa, ATM.
Wezi hao walichimba ukuta wa nyuma wa Benki hiyo na kutoweka na sanduku la uhifadhi wa pesa pamoja na mtambo wa ATM, pesa zikiwa ndani.
Washukiwa waliweza kuzima kamera za CCTV na pia kengele ya usalama kabla ya kutekeleza wizi huo.
Akizungumza na BBC, kamanda wa jimbo la Nairobi Japheth Koome amesema kwamba polisi waliweza kupata mitungi ya gesi na vifaa vingine ambavyo hutumuka kukata chuma.
Alipoulizwa kama wezi siku hizi wamepata maarifa utadhani wanaiga filamu, alisema kwamba kwa siku za hivi karibuni wizi wa benki unazidi kubadilika sana.
Mwaka uliopita, wezi waliojifanya wakaguzi wa hesabu katika benki hiyo walitoweka na dola za Marekani 300,000
SAMWEL SITTA HATUNAYE
Historia yake:
Samuel John Sitta alizaliwa Desemba 18, 1942 huko wilayani Urambo
Mkoa wa Tabora. Sitta alisoma Shule ya Msingi Urambo kati ya mwaka 1950
– 1953, kisha alikwenda Wilaya ya Sikonge mwaka 1954 - 1957 na
kuendelea na masomo ya “Middle School” katika shule ya “Sikonge Middle
School”. Baadaye mwaka 1958 – 1963 alianza masomo ya sekondari Shule ya
Wavulana Tabora yaani “Tabora Boys” kidato cha I – IV na cha V – VI.Mara tu baada ya kuhitimu masomo ya sekondari, Sitta alijiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kusomea Shahada ya Sheria (L LB) mwaka 1964 na kuhitimu mwaka 1971.
Ijumaa, 28 Oktoba 2016
MPIGA MBIZI AIBUA BOMU LA NYUKLIA
Bomu la nyuklia lililopotea
Mpiga mbizi mmoja huenda amegundua bomu la kinyuklia la Marekani ambalo lilipotea katika pwani ya Canada.
Sean Smyrichinsk alikuwa akiogelea akiwatafuta majongoo wa baharini karibu na Colombia inayomilikiwa na Uingereza wakati alipogundua chuma kikubwa kilichofanana na kisahani .
Idara ya ulinzi nchini Canada inaamini huenda ni bomu la kinyuklia kutoka kwa ndege ya kivita aina ya US B-36 Bomber ilioanguka katika eneo hilo 1950.
Serikali hiyo haiamini kwamba bomu hilo lina Nyuklia.
Canada tayari imetuma ndege ya wanamaji katika eneo hilo karibu na Haida Gwaii ili kulikagua bomu hilo.
TB Joshua: Bi Clinton atashinda urais Marekani
Muhubiri maarufu wa
vipindi vya Televisheni nchini Nigeria TB Joshua amesema ametabiri "
kwamba Hillary Clinton atamshinda Donald Trump" katika uchaguzi wa urais
wenye ushindani mkali tarehe 8 Novemba mwaka huu.
Katika ujumbe alioutuma kwenye ukurasa wake wa Facebook TB Joshua amesema kuwa Bi Clinton atashinda kwa ushindi mdogo, lakini atakabiliwa na changamoto nyingi - likiwemo jaribio la kupiga kwa kura ya kutokuwa na imani dhidi yake.
TB Joshua ni mmoja wa viongozi wa kidini wenye ushawishi na utata barani Afrika, huku wengi wa wafuasi wake wakiamini kuwa "utabiri " wake ni wa uhakika.
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA BALOZI WA HESHIMA WA TANZANIA NCHINI FINLAND
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akizungumza na Balozi wa Heshima wa Tanzania nchini Finland Mhe.
Vesa Viitaniem (kushoto), Ikulu jijini Dar es Salaam, katikati ni
Mwenyekiti wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote Mama Anna Mkapa .
Alhamisi, 27 Oktoba 2016
WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI WANNE KUTOKA NCHI MBALIMBALI, JIJINI DAR ES SALAAM LEO
Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akimkaribisha ofisini kwake
Balozi wa Norway nchini, Hanne-Marie Kaarstad (kushoto) kwa ajili ya
kufanya mazungumzo naye kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya
Norway na Tanzania. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Waziri
huyo, jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara
hiyo, Balozi Simba Yahya. Picha na zote Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi.
BREAKING NEWS DARASA LA SABA MATOKEO HAYA HAPA
BREAKING NEWSS:HAYA NDIO MATOKEO YA DARASA LA SABA
Kuyatazama matokeo ya darasa la saba mwaka 2016;
Bofya Hapa au
WAZIRI MAKAMBA AKAMILISHA ZIARA KATIKA MKOA WA KATAVI
Bibi
Josephine Rupia, Mkuu wa Idara ya Maliasili Halmashauri ya Mpanda
akitoa maelezo ya Mto Katuma kupoteza mwelekeo wa kutiririsha maji
katika mkondo wake kama ilivyokuwa hapo awali.
Wengine katika picha ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga
Wengine katika picha ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)