Katika karibu kila 
jambo duniani, mwanadamu huhitajika kutumia akili ili kufanikiwa. Bila 
shaka, iwapo utatarajia uwazidi watu wengine hasa katika kuwapora au 
kuwaibia basi utahitajika kuwa na ujanja zaidi. Lakini maeneo mbalimbali
 duniani kunao wahalifu ambao walionekana kupungukiwa.
Majuzi kwa 
mfano, wanaume wawili kutoka Skegness, Lincolnshire, walijipiga picha 
wakiiba pesa kutoka kwenye mitambo ya kucheza Kamari Bradford, 
Uingereza. Hawakuenda mbali, kwani walikamatwa muda mfupi baadaye 
Benjamin Robinson, 30, alifungwa jela miezi 32, naye Daniel Hutchinson 
akahukumiwa kifungo cha miezi sita jela ambacho kimeahirishwa.
Hawako peke yao. Hapa ni msururu wa wahalifu wengine waliojichongea:
1. Jambazi aliyejitapa Facebook
Andrew
 Hennells alikamatwa baada yake kuandika kwenye Facebook akijisifu 
kuhusu mpango wake wa kushambulia duka la jumla la Tesco eneo la King's 
Lynn, Norfolk.