Mwanamke ambaye
alishambuliwa na mmewe na kukatwa mikono nchini Kenya, baada ya ndoa yao
kuvunjika kwa kishindwa kuzaa mtoto, sasa anaripotiwa kuwa mjamzito.
Muda
mfupi baada ya kushambuliwa, Jackline Mwende alisema kuwa madaktari
walikuwa wamewajulisha kuwa yeye alikuwa na uwezo wa kushika mimba,
lakini mmewe Stephen Ngila, hakuwa na uwezo wa kuzaa.Kwenye mahojiano na gazeti na Daily Nation, Mwende amesema kuwa hali hii ilichangia aanze uhusiano mwingine nje ya ndoa.
Anasema alikuwa na haja ya kuwa na watoto ndipo akaanza uhusiano na mwanamume mwingine ili kuokoa ndoa yake, lakini mumewe ambaye sasa anakabiliwa na kesi ya kutaka kuua akagundua.
"Nilikuwa ninataka mtoto. Nilikuwa na haja ya mtoto...na pia ibilisi alisababisha mimi kutembea nje ya ndoa yangu. Haikuwa vizuri kufanya hivyo, ninajua watu watanihukumu vikali kwa sababu ya hilo. Kwa vile niko hai na nitajifungua mtoto hivi karibuni, nina matumaini licha ya kupitia taabu." Alisema Bi Mwende.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni