UNYAMA MKUBWA: BINTI WA MIAKA 16 ACHINJWA SINGIDA
 
Kamanda wa 
Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela 
WATU wasiojulikana wilayani 
Manyoni wamemchinja mithili ya kuku binti mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa 
miaka 16. 
Diwani 
wa Kata ya Manyoni Mjini, Hamis Masabuni alisema tukio hilo lilitokea juzi 
asubuhi katika eneo la Mitoo kwenye mashamba ya Magereza, Uwanja wa Ndege wa 
zamani. 
Alisema siku ya tukio, yeye alipata taarifa ya simu kutoka kwa 
raia wema hivyo ikambidi aende huko kushuhudia kulikoni na mara alipofika eneo 
hilo alikuta mwili wa marehemu ukiwa umelala chini na kuchinjwa mithili ya kuku. 
Diwani huyo amelitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina juu ya 
tukio hilo ili kubaini wauaji wa binti huyo ili hatua za kisheria ziweze 
kuchukuliwa dhidi yao. 
Muuguzi wa zamu katika hospitali ya wilaya ya 
Manyoni, Getruda Njughuda amekiri kuupokea mwili wa binti huyo. 
Naye 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela alisema kuwa polisi 
inaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo.HABARILEO.
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni