Jumanne, 16 Juni 2015

AJALI YAUA 23 MAFINGA

 
Na Berdina Majinge

Basi hilo, lifanyalo safari zake kati ya Iringa na Njombe, lilipata ajali hiyo saa 1:45 usiku wa kuamkia jana wakati dereva alipokuwa akijaribu kuyapita magari mengine kabla ya kugongana uso kwa uso na lori.
Watu 23 wamekufa papo hapo na wengine 34 kujeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya Another G kugongana na lori eneo la Kinyanambo A, Mafinga wilayani Mufindi, ikiwa ni takriban miezi mitatu baada ya ajali nyingine iliyoua watu 50 katika wilaya hiyo.
Basi hilo, lifanyalo safari zake kati ya Iringa na Njombe, lilipata ajali hiyo saa 1:45 usiku wa kuamkia jana wakati dereva alipokuwa akijaribu kuyapita magari mengine kabla ya kugongana uso kwa uso na lori.
Kaimu kamanda wa polisi wa Mkoa wa Iringa, Pudenciana Protas alisema basi hilo lilikuwa likiendeshwa na Nicholaus Mangula (29) na lori la Kampuni ya Bravo Logistics lililokuwa likiendeshwa na Rogers Mdoe (39) na ambalo lililikuwa likitokea Zambia kuelekea Dar es Salaam.
Katika ajali hiyo, dereva wa lori alifariki dunia papo hapo.
Machi 10 mwaka huu, watu 50 walipoteza maisha kwenye ajali iliyotokea Mafinga, Changarawe, wakati kontena lililokuwa limebwa na lori lilipochomoka wakati dereva akijaribu kukwepa mashimo barabarani na kuangukia kwenye lori.
Alisema majeruhi wamelazwa Hospitali ya Wilaya ya Mufindi mjini Mafinga na maiti zimehifadhiwa hospitalini hapo ikiwamo ya dereva wa lori aliyekufa papo hapo.
Alisema chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa basi la Kampuni ya Another G ambaye alikuwa kwenye mwendo kasi na alikuwa akiyapita magari mengine bila tahadhari ndipo alipofika katikati alikutana na lori na kuamua kulichepusha nje ya barabara hali iliyosababisha kupinduka na kisha lori kuligonga basi hilo ubavuni.
Alisema baada ya ajali hiyo, dereva wa basi alikimbia lakini polisi wamemkamata na yupo chini ya ulinzi.
Waliokufa na kutambuliwa mpaka sasa ni Lukas Pascal, Brasto Samila, Dickson Luvanda, Albert Silla, Rogers Mdoe, Eva Mbalinga, Hadija Mkoi, Clemence Mtati, Mohamed Kalika, Kastoli Mwakyamba, Damian Myala na Sillo Nziku.
Waliojeruhiwa ni Majoline Lupembe (23) mkazi wa Iringa, Veronica Simba (20, Tabora), Shadia Ally (24, Iringa), Mariam Mbise (23, Mafinga), Anita Makwela (24, Kilolo), Benita Sagala (18, Njombe), Bertha Mkoi (27),  Rahel Mavika (18, Mufindi), Selina Fulgence (23, Kigoma) na  Maria Mwenda (17) mkazi wa Mafinga.
Majeruhi wengine ni Ndipako Mbilinyi (23, Njombe), Alexander Mkakazii (28, Mafinga), Meshack Kibiki (44, Mafinga), Simon Jumbe (22, Singida), Jerry Lutego (36, mkazi wa Mafinga), Enock Kanyika (18, Mafinga), Deogratius Kayombo (21, Mafinga) na Yusuph Lulanda (22) mkazi wa Njombe.
Wengine waliojeruhiwa ni Petro Mwalongo (21, Njombe), Paulo Chane (21, Kilolo), Kenned Msemwa (28, Njombe), Mode Shiraz (21, Singida), Emmanuel Antony (21, Mwanza), Godfrey Kanyika (39, Mafinga) na Boniface Bosha (20).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni