Ijumaa, 10 Juni 2016

Wakili apigwa na kuchaniwa nguo mbele ya majaji China

Wakili wa China aliyepigwa na kuchaniwa nguo akitoka mahakamani
Mawakili wengi wa China wamenyanyaswa, kukamatwa na hata kufungwa jela lakini picha ya mmoja wao aliyekuwa na nguo zake zilizochanwa na maafisa wa polisi imevutia hisia nyingi nchini China.

Wu Liangshu alikuwa katika mahakama ya wilaya ya Qingxiu akiwa amevalia koti lake na suruali nyeusi akiwa mtanashati kabisa lakini alipotoka alikuwa hana koti na suruali yake kuchanwa hadi nguo ya ndani ikionekana.

Yeye na mawakili wengine waliwaambia maafisa wa mahakama kwamba alishambuliwa na maafisa watatu katika mahakama moja mbele ya majaji wawili ambao walikataa ombi lake la kutaka kuanzisha kesi katika mahakama ya wilaya ya Nanning Mkoani Guangxi.

Bw Wu alipewa nguo nyengine lakini alijua uwezo wa kile alichokuwa akipanga kukifanya.''Asante alisema''.
Wakili huyo baadaye alitembea kupitia mlango wa mbele akiwa amebeba nakala zake za mahakamani akiwa na kalamu iliowekwa katika mfuko wa shati liliposuliwa.

Baadaye alipigwa picha nje ya jengo hilo la mahakama na picha hiyo kusambazwa. Hii ilikuwa na maana ya kutuma ujumbe kewa nchini China mawakili wananyanyaswa. Meseji sent

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni