Jumamosi, 18 Juni 2016

JK KUENDELEA KUPAA: ATEULIWA KUWA BALOZI WA HESHIMA

Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea barua ya uteuzi kutoka kwa Prof. Kamuzora alipofanya ofisi za CCM Lumumba
 Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na  Prof. Kamuzora alipofanya ofisi za CCM Lumumba

KITUO cha Ufundi cha Kilimo na Maendeleo Vijijini (Technical Centre for Agricultural and Rural Cooperation, CTA) kilicho chini ya Umoja wa Ulaya (EU) chenye makao makuu mjini Wageningen, Uholanzi kimemteua Rais Mstaafu Dk. Jakaya  Kikwete kuwa Balozi wa Heshima (Goodwill Ambassador) wa Maendeleo ya Kilimo katika Mabara ya Afrika, Caribean na Pacific.
Katika barua iliyokabidhiwa na mjumbe wa Bodi ya CTA, Prof. Faustin Kamuzora, CTA wameainisha kuwa Dk. Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, ameteuliwa kwa kutambua mchango na juhudi zake katika kukiendeleza kilimo nchini Tanzania na barani Afrika.
Katika wadhifa wake huo mpya, CTA imemuomba Dk.  Kikwete aweze kuiwakilisha katika makongamano ya kimataifa ambapo atazungumzia umuhimu wa kukiendeleza kilimo kwa ajili ya kutoa fursa ya ajira zenye staha na uhakika kwa vijana na wanawake katika nchi za barani Afrika, Karibiani na Pasifiki. Pia ataisaidia CTA katika kuandaa makala na kufanya mahojiano na waandishi wa habari katika nchi mbalimbali.
Dk. Kikwete amekubali uteuzi huo na kuahidi kushirikiana na CTA katika kutekeleza mambo ambayo ameombwa kuisaidiana na taasisi hiyo ambayo ni ya ushirikiano wa Umoja wa Ulaya na Kundi la nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki wenye makao makuu mjini Brussels, Ubelgiji.
Prof. Kamuzora ambaye pia ni Katibu Mkuu, Mawasiliano ni mjumbe wa Bodi ya CTA akiwakilisha nchi za ukanda wa Afrika Mashariki kwa miaka mitano tangu 2013 hadi 2018

Ijumaa, 10 Juni 2016

WATOTO SITA WAFA UBATIZONI ZIMBABWE

 
 Robert Mugabe
Watoto sita wamekufa maji bila kutarajiwa katika sherehe za kubatizwa kwao katika mto nchini Zimbabwe. Watoto watatu walinusurika kufa maji ya mto huo ambao maji yake ni ya baridi; watoto hao walionekana wakitetemeka kutokana na baridi wakati miili ya wenzao waliokufa maji ikiopolewa majini.

Polisi nchini Zimbabwe wamewatia mbaroni watu wawili ambao ni wafuasi wa dhehebu moja la Kikristo.

Pia walisema kuwa wamemkamata mama mmoja ambaye alidai kwamba yeye ni nabii na ambaye alisema kwamba alifanya jaribio la kufufua wafu wakati wa ibada zake.

Wakili apigwa na kuchaniwa nguo mbele ya majaji China

Wakili wa China aliyepigwa na kuchaniwa nguo akitoka mahakamani
Mawakili wengi wa China wamenyanyaswa, kukamatwa na hata kufungwa jela lakini picha ya mmoja wao aliyekuwa na nguo zake zilizochanwa na maafisa wa polisi imevutia hisia nyingi nchini China.

Wu Liangshu alikuwa katika mahakama ya wilaya ya Qingxiu akiwa amevalia koti lake na suruali nyeusi akiwa mtanashati kabisa lakini alipotoka alikuwa hana koti na suruali yake kuchanwa hadi nguo ya ndani ikionekana.

Yeye na mawakili wengine waliwaambia maafisa wa mahakama kwamba alishambuliwa na maafisa watatu katika mahakama moja mbele ya majaji wawili ambao walikataa ombi lake la kutaka kuanzisha kesi katika mahakama ya wilaya ya Nanning Mkoani Guangxi.

Bw Wu alipewa nguo nyengine lakini alijua uwezo wa kile alichokuwa akipanga kukifanya.''Asante alisema''.
Wakili huyo baadaye alitembea kupitia mlango wa mbele akiwa amebeba nakala zake za mahakamani akiwa na kalamu iliowekwa katika mfuko wa shati liliposuliwa.

Baadaye alipigwa picha nje ya jengo hilo la mahakama na picha hiyo kusambazwa. Hii ilikuwa na maana ya kutuma ujumbe kewa nchini China mawakili wananyanyaswa. Meseji sent

Ijumaa, 3 Juni 2016

Video yawatia matatani wanafunzi waliofanya mtihani India

 
Bihar wazazi wakipanda kuta kusaidia watoto wao
Wanafunzi 14 walioongoza katika matokeo ya mtihani wa mwisho katika jimbo la Bihar nchini India watalazimika kufanya tena mtihani kufuatia madai kwamba walihusika na udanganyifu, serikali ya jimbo hilo imsema.
Uamuzi huo uliafikiwa baada ya mmoja ya wanafunzi hao Ruby Rai mwenye umri wa miaka 17 kuviambia vyombo vya habari kwamba sayansi ya siasa inahusisha kupika.

Jumatatu, 30 Mei 2016

SHEKHE AUAWA KATIKA FUMANIZI

JESHI la Polisi Wilaya ya Tunduru, mkoani Ruvuma, linamshikilia mkazi wa Kijiji cha Likweso, Tarafa ya Mchoteka, Ally Mchumwa
kwa tuhuma za mauaji ya Shekhe wa kijiji hicho.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Zubery Mwombeji, alisema tukio hilo limetokea Mei 22, mwaka huu, baada ya mtuhumiwa (Mchumwa), kumfumania akifanya tendo la ndoa na mkewe.

"Mauaji haya yametokea saa tatu asubuhi wakati marehemu ambaye amefahamika kwa jina la Seleman Mwalabu (45), mtuhumiwa na mkewe Mariamu Husein, wakisaidiana kuvuna njugu shambani.

"Wakati wakiendelea na kazi hiyo, mtuhumiwa alitoka kidogo na kumuacha marehemu pamoja na mkewe wakiendelea na kazi hiyo, aliporejea hakuwakuta shambani hivyo akashtuka," alisema.

Kamanda Mwombeji alisema wakati mtuhumiwa akiwa katika kwenye sintofahamu hiyo, alisikia sauti ikitoka porini jirani na shamba lake hivyo aliamua kwenda na kumkuta mkewe na mtuhumiwa wakiwa uchi wa mnyama ikiashiria wametoka kufanya tendo la ndoa.

Kutokana na hali hiyo, mtuhumiwa alichomoa kisu na kumchoma nacho marehemu shingoni, kufariki papo hapo na yeye mwenyewe akajisalimisha kwa uongozi wa Serikali ya kijiji na baadaye kupelekwa polisi.

Aliongeza kuwa, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani ili sheria iweze kuchukua mkondo wake baada ya uchunguzi kukamilika

SAMATTA AIPELEKA GENK EUROPA LEAGUE


Tarehe May 29, Mbwana Samatta ameandika historia mpya kwenye maisha yake baada ya kuisaidia timu yake ya Genk kushinda mchezo wa fainali ya play off na hatimaye kufuzu kucheza michuano ya Ulaya (Europa League).
Samatta ambaye alianza kwenye kikosi cha kwanza cha Genk ameisaidia klabu yake kupata ushindi wa magoli 5-1 kwenye uwanja wao wa nyumbani (Cristal Arena) dhidi ya Sporting Charleroi.

Alhamisi, 19 Mei 2016

DOLA ZA KIMAREKANI BILIONI 3 KUTUMIKA KUANZISHA MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (kushoto) akiongea na Waandishi wa Habari (hawako pichani) kuhusu kuanza kwa mradi wa Mgodi wa kuchimba chuma na makaa ya mawe Liganga na Mchuchuma leo mjini Dodoma 19 Mei, 2016. Katikati ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayosimamia viwanda, biashara na uwekezaji, Mhe. Dkt. Dalaly Kafumu pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji toka Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Bwana Mlingi Mkucha.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayosimamia viwanda, biashara na uwekezaji, Mhe. Dkt. Dalaly Kafumu (kulia) akisisitiza jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawako pichani) kuhusu kuanza kwa mradi wa Mgodi wa kuchimba chuma na makaa ya mawe Liganga na Mchuchuma leo mjini Dodoma 19 Mei, 2016. Kushoto ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage.


Na Benedict Liwenga, MAELEZO, Dodoma.

JUMLA ya dola Bilioni 3 za Kimarekani zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa Mgodi wa Makaa ya Mawe na Chuma wa Liganga na Mchuchuma.Kauli hiyo imetolewa Leo mini Dodoma na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage wakati akiongea na Waandishi wa habari mini Dodoma.

Jumatatu, 16 Mei 2016

Lidege likubwa zaidi duniani latua Australia

Antonov An-225 Mriya ndiyo ndege refu na nzito zaidi kuwai kujengwa.
Maelfu ya watu nchini Australia wanaopenda ndege walikusanyika kutizama ndege kubwa zaidi duniani ya Antonov An-225 Mriya, ilipowasili mjini Perth nchini humo.
Ndege hiyo yenye urefu wa mita 84 na uzito wa tani 175 bila ya kubeba mzigo wala mafuta, ilikuwa ikisafirisha jenereta yenye uzito wa tani 117.

KITISHO CHA BOMU CHAAHIRISHA MECHI YA MAN U

 
 Hofu ya kuwepo bomu uwanjani imesababisha mechi ya Manchester United na Bournemouth kuahirishwa.

Mechi ya mwisho katika ligi ya soka ya uingereza, EPL, kati ya Manchester united na Bournemouth imeahairishwa kufuatia wasiwasi wa bomu, uwanjani Old Trafford.

Jumatatu, 18 Aprili 2016

TETEMEKO LAUA WATU 272 ECUADOR

Rescue workers search the rubble of a collapsed building for victims in Guayaquil, Ecuador, on Sunday, April 17. A magnitude-7.8 quake struck off Ecuador's central coast on Saturday, April 16, flattening buildings and buckling highways. It's the deadliest quake to strike the South American country in decades.
Tetemeko kubwa la ardhi lenye ukubwa wa 7.8 katika vipimo vya Ritcher limeikumba nchi ya Ecuador na kuua watu wapatao 272 na kujeruhi wengine 2500.

Tetemeko hilo ni kubwa na limekumba maeneo ya pwani ya nchi hiyo.

Juhudi za uokozi zinaendelea.