Mkuu wa mkoa akimpeleka Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro na Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mh  Innocent Kalogeris  kupokea mwili wa mpendwa mke wake,kulia ni dada wa mbunge huyo.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh Dr Joel Bendera Leo amewaongoza mamia ya wananchi wa mkoa wa Morogoro kumzika Mke wa Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini, Mh lnocenti Kalogeris watu mbali mbali wakiwemo wabunge,wakuu wa mikoa wa staafu na watu mashuhuri wamefurika nyumbani kwa mbunge huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Morogoro CCM 
 Marehemu Elizabeth Kapoloma enzi za Uhai wake, Bi, Elizabeth Kapoloma alifariki Alhamisi Kwa Ugonjwa Moyo.
 Mwili wa marehemu ukiwasili nyumbani kwake kwajili ya Heshima za Mwisho na Ibada kabla ya Mazishi 
  Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mh Dk Joel Bendera akimbembeleza Mume wa marehemu Mhe lnocent Kalogeris
 Mbunge huyo akiingizwa kwenye chumba kilichowekwa jeneza lenye mwili wa mpendwa mke wake.
 Diwani wa Kata ya Mji Mpya Wensislaus Karogerezi ambaye ni kaka wa mbunge huyo akiangua kilio kwa uchungu baada ya kuondokewa na shemeji yake mpendwa 
 Mstakihi Meya wa Mji wa Morogoro Amir Juma Nondo ambaye pia ni Diwani wa kata ya Boma akimbembeleza Diwani mwenzake  Wensislaus Kalogeris  ambaye ni Kaka wa Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini
 Mtoto wa Marehemu akiangua kilio baada ya mwili wa mpendwa mama wake kuwasili nyumbani kwao 
                 Mbunge wa viti maalumu'CCM'  Mhe Magreth Mkanga
 Mbunge mstaafu wa jimbo la Morogoro Kusini Mashariki Lotto akimpa pole Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mh lnnocent Kalogeris Kwenye mazishi ya Mkewa Mbunge huyo.
Mbunge wa Jimbo la Morogoro  Mhe  lnnocent Kalogeris akifarijiana na mama yake mzazi 
Na Dustan Shekidele,Morogoro
 













