Taarifa zlizotufikia hivi punde ni kuwa moto mkubwa umezuka katika Jengo D lililopo ndani ya Mabibo Hostel zinazomilikiwa na kuendeshwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Shuhuda aliyekuwa eneo la tukio ametujuza kuwa Askari wa Zimamoto wamechelewa kufika na athari zilishaanza kuwa kubwa, jitihada za kuuzima moto huo zinaendelea.
Chanzo bado hakijafahamika!
Jumatatu, 16 Machi 2015
BREEEKING NEWWZZZZ: Moto wazuka Hosteli za Mabibo
MAANDAMANO MAKUBWA MONDULI: WANANCHI WAMWOMBA LOWASSA AGOMBEE URAIS
makundi mbalimbali ya kijamii ya mikoa ya Kaskazini, inayojumuisha mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Arusha na Manyara wakiwa wanaandamana kwa pamoja kuelekea kwa mbunge wa jimbo la monduli  hii leo
Katibu wa
 Chama cha Wasioona Mkoa wa Kilimanjaro  (TLB), Protas Soka Akisoma 
risala kwa niaba ya makundi hayo mbele ya mbunge wa jimbo la Monduli
Jumapili, 15 Machi 2015
IKO SIKU NITAKUWA MTU MKUBWA - ZITTO
Zitto: Iko siku nitashika nafasi kubwa Tanzania
            
Wananchi wa Kijiji cha Nyalubanda wakiwa wamembeba Mbunge wa Kigoma 
Kaskazini, Zitto Kabwe alipowasili katika kijiji hicho jana katika hafla
 ya kukabidhi gari la wagonjwa alilotoa ahadi katika kampeni za Uchaguzi
 wa mwaka 2010. Picha na Edwin Mjwahuzi 
            
    Na Antony Kayanda na Saumu Mwalimu, Mwananchi
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe 
amesema kutimuliwa uanachama na Chadema ni dhoruba inayomkumba 
mwanasiasa yeyote anayefanikiwa na kwamba iko siku atashika “nafasi 
kubwa ya uongozi ya kuwatumikia Watanzania”.
Zitto aliwasili mjini hapa juzi, ikiwa ni siku 
chache baada ya Chadema kutangaza kumtimua uanachama kwa kosa la 
kupeleka mgogoro wa ndani ya chama kwenye mahakama.
Alifungua kesi Mahakama Kuu akitaka imuamuru 
katibu mkuu wa Chadema kumpa nyaraka za mwenendo wa vikao vya Kamati Kuu
 vilivyomvua madaraka yote na baadaye kukizuia chama hicho kumjadili. 
Hata hivyo mahakama ilitupilia mbali shauri lake na Chadema ikatangaza 
mara moja kumtimua.
Akihutubia mamia ya watu kwenye Kijiji cha 
Nyarubanda ambako alikabidhi gari la wagonjwa, Zitto aliwatoa hofu 
wananchi hao walioonyesha shauku ya kujua hatma yake na kuwaeleza kuwa 
hajawatupa, ataendelea kuwahudumia.
“Hakuna kiongozi aliyefanikiwa kisiasa bila 
kupitia misukosuko ya kupingwa,” alisema Zitto ambaye anamalizia kipindi
 cha pili cha ubunge wake kwenye jimbo hilo.
“Waziri Mkuu za zamani ya India, Indira Gandhi 
alifukuzwa na chama chake na aliamua kuunda chama kipya na baadaye 
kuwashinda waliomfukuza katika uchaguzi. Kwa hiyo nawatoa hofu kwa maana
 ninajengwa zaidi kisiasa.
“Nipo kwenye dhoruba ambayo inanijenga kisiasa na 
ipo siku nitawatumikia Watanzania katika nyadhifa kubwa za uongozi.” 
Katika mkutano huo ambao wananchi walimpokea wakiwa na mabango yenye 
ujumbe mbalimbali kama “Mheshimiwa Zitto tulikuchagua wewe na siyo 
chama,” huku mengine yakiandikwa “chama siyo bora, ubora ni utendaji 
kazi”.
Viongozi mbalimbali wa CCM na vyama vingine vya 
siasa walijumuika kwenye uwanja huo kumpokea Zitto na kushiriki naye 
kucheza ngoma za asili.
Baadhi ya viongozi hao ni mwenyekiti wa 
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Hamisi Betese, mkurugenzi wa halmashari
 hiyo, Michael Mwandezi na viongozi wengine wa serikali za mitaa.
Akiongea katika hadhara hiyo, Betese alisema kuwa 
kitendo cha Zitto kutoa gari ambayo aliwaahidi wananchi kipindi cha 
uchaguzi ni utekelezaji wa ilani ya CCM ambayo ndiyo chama tawala.
Aliongeza kuwa yeye kama mwenyekiti wa halmashauri
 bado anamtambua Zitto kama mbunge wa Kigoma Kaskazini mpaka hapo 
taarifa rasmi zitakapotolewa.
Wanakijiji hao walishukuru Zitto kwa kutoa gari 
hilo wakisema litawasaidia kuokoa fedha nyingi walizokuwa wakitumia 
kutafuta magari binafsi wanapokuwa na wagonjwa wanaohitaji matibabu ya 
haraka.
VATICAN YASEMA KUNA HAJA YA KUTUMIA NGUVU DHIDI YA IS
Askofu mkuu wa Vatican Silvano Tomasi
 Makao makuu ya kanisa katoliki duniani Vatican yanasema kuwa nguvu 
inaweza kutumiwa kusitisha mashambulizi yanayoendeshwa na wanamgambo wa 
Islamic State dhidi ya wakristo na makundi mengine madogo .
Askofu
 mkuu Silvano Tomasi ambaye ni mwakilishi mkuu wa Vatican kwenye umoja 
wa mataifa mjini Geneva ameyashutumu makundi ya jihad kwa kuendesha 
mauaji ya halaiki.Akizungumza kupitia mtandao wa Vatican amesema kuwa hatua za kijeshi zitaanzishwa ikiwa suluhu ya kisiasa haitapatikana.
Lakini amesema kuwa muungano wowote dhidi ya Islamic State ni lazima ujumuishe nchi za kiislamu kutoka mashariki ya kati.
WENGER ASEMA ARSENAL ITAIFUNGA MONACO
kocha wa arsenal Arsene Wenger
Kocha
 wa Arsenal Arsene Wenger anaamini kuwa kilabu hiyo bado ina fursa ya 
kuibandua Monaco katika michuano ya kilabu bingwa barani Ulaya licha ya 
kucharazwa 3-1 katika awamu ya kwanza ya mechi hizo.
Arsenal 
itakabiliana na timu hiyo ya Ligi ya daraja la kwanza siku ya jumapili 
huku ikiwa hakuna timu ilioweza kufanikiwa kubadilisha matokeo kama hayo
 katika michuano hiyo.Wenger:Tuna changamoto kubwa mbele yetu lakini tutafanya kila kitu kuhakikisha kwamba tunafuzu kwa robo fainali.
''Wao ndio wanaopigiwa upato kufuzu lakini tunaweza kubadilisha mambo''.
''Tutahakikisha kuwa tuna hamu na imani ya kushinda''.
Tayari kilabu hiyo imepata motisha kufuatia ushindi wao wa mabao 3-0 dhidi ya kilabu ya West Ham siku ya jumamosi. .
MABOMU YALENGA MAKANISA PAKISTANI
 Mabomu mawili yamelipuka yakilenga makanisa mawili yaliyokuwa yamejaa 
watu kwenye mji wa Lahore chini Pakistan wakati watu walipokuwa 
wakihudhuria misa ya jumapili.
Polisi wanasema kuwa takriban watu 6 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa.Mashambulizi hayo yanaoyoaminika kuwa ya kujitoa mhanga yalifanyika eneo lenye waumini wengi wa kikristo la Youhanabad
UGIRIKI YAONYA KUHUSU KUONDOLEWA KATIKA KANDA SARAFU YA EURO
Ugiriki imesema kama taifa hilo litakuwa kwenye hatua ya kuondoka katika
 kanda ya mataifa yanayotumia sarafu ya Euro, basi mataifa ya Uhispania 
na Italia yanaweza kufuata mkondo huo.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ulinzi wa Ugiriki, Panos Kammenos, 
wakati akizungumza na gazeti la Ujerumani la Bild, katika mahojiano 
ambayo yatachapishwa leo Jumamosi (14.03.2015). Kammenos amesema kama 
Ugiriki ikiondoka kwenye kanda inayotumia sarafu ya Euro, basi Uhispania
 na Italia zitafuata, na hata ikiwezekana Ujerumani pia.WAKURDI WAPATA USHUNDI MUHIMU DHIDI YA DOLA LA KIISLAMU
Wapiganaji wa Kikurdi na wanamgambo wa kikristo wanapata mafanikio 
katika mapigano dhidi ya magaidi wa "Dola la Kiislamu" Kaskazini 
Mashariki mwa Syria. Hata hivyo pana taarifa juu ya mapigano makali.
Kwa mujibu wa taarifa ya afisa mmoja wa kikurdi na asasi ya 
wanaharakati, katika mapambano dhidi ya kundi linaloitwa Dola la 
Kiislamu, wapiganaji wa kikurdi wanaoshirikiana na wanamgambo wa 
Kikristo, wanapata mafanikio.Afisa huyo Nasser Haj Mansour kutoka wizara ya ulinzi katika jimbo la wakurdi la nchini Syria, amesema wapiganaji wa kikurdi wamekiteka kijiji kimoja katika jimbo la Hassakeh ambacho hapo awali kilikuwa kinadhibitiwa na wapiganaji wa Dola la Kiislamu.
Afisa huyo pamoja na wawakilishi wa asasi inayofuatilia haki za binadamu nchini Syria kutokea London, wamesema wapiganaji wa Peshmerga walikiteka kijiji hicho usiku wa juzi.
Ijumaa, 6 Machi 2015
MAAFA KAHAMA: SERIKALI YAANZA KUCHUKUA HATUA


Kufuatia mvua kubwa zilizonyesha usiku wa
 tarehe 04 Machi, 2015 Wilayani Kahama mafuriko makubwa yalitokea na 
kuathiri wakazi wa kata ya Mwakata katika vijiji vya Mwakata, Numbi na 
Mwaguguma. Kutokana na mafuriko yaliyotokea tathmini ya awali inaonesha 
kuwa watu 42 wamepoteza maisha, watu 82 wamejeruhiwa na watu 
wanaokadiriwa kufikia 574 wameathirika. Jumla ya nyumba 137 zimeathirika
 kwa viwango mbalimbali.
Serikali imechukua hatua za haraka kwa 
kushirikiana na wananchi kuwafikia na kuwanusuru waathirika wa mafuriko 
hayo waliokuwa wamezingirwa na mafuriko. Aidha vimeanzishwa vituo vya 
muda kuwahifadhi wananchi hao kwenye Shule.
Serikali imepeleka misaada ya kibinadamu kama ifuatavyo;
i. Chakula tani 20. Maharage tani 5, Mafuta ya kupikia lita 1,126 na Sukari tani 1.3
ii. Vifaa vya matumizi ya ndani ambayo 
vinajumuisha blanketi 650, ndoo 82 za lita 20, ndoo 82 za lita 10 ; 
Vifaa vya kupikia seti 82 na madumu 82
Kwa kuwa bado Serikali inalo jukumu kubwa
 la kuwawezesha waathirika kurejea katika maisha yao ya kawaida; 
inapenda kuwatangazia wale wote wanaoguswa na maafa haya kuwa Serikali 
inaendelea kupokea misaada mbalimbali ambayo inahitajika kwa waathirika.
Mahitaji haya ni pamoja na sare za shule;
 daftari za wanafunzi; mavazi ya kike na kiume; na chakula. Aidha kwa 
kuzingatia kuwa waathirika hawa wamepoteza mali na fedha katika maafa 
haya; misaada ya vifaa vya ujenzi (sementi, mabati, mbao, n.k.) 
inahitajika sana.
Utaratibu wa kupokea misaada hiyo kwa 
walio Dar es Salaam wanaweza kuiwasilisha misaada hiyo Idara ya Kuratibu
 Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu au kuwasiliana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa 
Shinyanga.
Serikali itaendelea kuwasaidia Waathirika
 dhidi ya Changamoto zinazoweza kujitokeza hususani za kiafya 
zinazosababishwa na uchafuzi wa vyanzo vya maji na mazingira. Elimu juu 
ya ujenzi wa nyumba bora na makazi maeneo salama itaendelea kutolewa.
Alhamisi, 5 Machi 2015
FORD YAGEUkIA BAISKELI
baiskeli inayotumia umeme
Kampuni
 ya kutengeza magari ya Ford imezindua baiskeli ya kielektroniki kwenye 
mkutano mkubwa wa magari duniani katika mpango wake wa upanuzi.
Kampuni
 zaidi za kutengeza magari zinatafuta njia mbadala za kutengeza pesa 
huku nyingi zikitengeneza kile kinachoitwa kama uchukuzi wa haraka.Baiskeli hizo zinazotumia umeme ziko aina mbili, moja inayotumiwa na wasafiri na nyingine inayotumiwa kufanya biashara.
Baiskeli zote mbili zina programu za smartphone zinazoweza kumuelekeza anayeziendesha.
Jaribio la baiskeli hizo ni miongoni mwa mipango ya kampuni ya Ford kubuni mbinu mpya ya usafiri huku ikifanya utafiti kuhusu jinsi baiskeli hizo zinzovyoweza kuingiliana na magari pamoja na usafiri wa uma.
''Kuna mbinu nyingi za kuzunguka mjini. Lakini kile kinachohitajika ni njia za kuunganisha mbinu hizi zote za usafiri pamoja amesema Ken Washington'', makamu wa rais wa kitengo cha utafiti cha Ford
WATU WANNE KUNYONGWA HADI KUFA MWANZA
Mahakama
 kuu ya Tanzania Mwanza  imewahukumu adhabu ya kunyongwa hadi kufa 
washtakiwa wanne akiwemo mume wa marehemu baada ya kupatikana na hatia 
ya kumuua zawadi Mangidu [22] wa kijiji cha Nyamalulu kata ya Kaseme 
wilayani Geita.
Hukumu hiyo imetolewa na Jaji Joaquine De-Mello 
katika ukumbi uliokuwa umefurika wasikilizaji wakiwemo ndugu wa upande 
wa washtakiwa na baada ya kutolewa hukumu baadhi ya ndugu wa washtakiwa 
walitokwa na machoziWaliohukumiwa adhabu ya kunyongwa hadi kufa ni Masalu Kahindi[54]Ndahanya Lumola[42]Singu Nsiyantemi[49]na Nassor Said[47] ambaye alikuwa mume wa marehemu Zawadi Mangindu wote wamepatikana na hatia ya kula njama na kushiriki kumuua zawadi kwa kukusudia ambaye alikuwa mlemavu wa ngozi.
Katika hukumu yake Jaji De-mello alisema alikuwa amezingatia kwa makini na tahadhari kubwa katika kufikia uamzi huo baada ya kupitia ushahidi wa upande wa mashtaka ambapo mashahidi 12 waliitwa na kutoa ushahidi pamoja na ule wa Utetezi na kisha kujiridhisha kuwa pasipo kuacha shaka yoyote washtakiwa walitenda kosa hilo.
ANAOGOPA KUISHI NJE YA KITUO
Mtoto Hassan Khamis ni miongoni mwa walemavu wa ngozi wanaohifadhiwa 
kwenye kituo cha Buhangija nchini Tanzania na sasa akiwa ameshakuwa 
mkubwa na kulazimika kutoka hapo, anasema hana uhakika wa maisha yake.
Katika mfululizo huu wa ripoti maalumu mwezi mzima kuangazia masaibu, 
changamoto na maisha wanayopitia watu wenye ulemavu wa ngozi, maarufu 
kama albino, ambao hivi karibuni wamekuwa wakilengwa na kushambuliwa 
nchini Tanzania kwa imani za kishirikina, hapa Idhaa ya Kiswahili ya DW 
inazungumza na kijana Hassani mwenye umri wa miaka 17 sasa na ambaye 
amehifadhiwa katika kituo cha Buhangija kinachowashughulikia watu 
wanaoishi na ulemavu wa ngozi mjini Shinyanga, Tanzania.Kusikiliza mahojiano na kijana Hassani, tafadhali bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.
Mwandishi: Amina Abubakar
WATANO WAUAWA KWA KUTUHUMIWA KUZUIA MVUA MKOANI MARA
Jeshi la 
polisi mkoa wa Mara limewakamata watu  saba wakiwemo viongozi wawili wa 
Serikali  ya  kijiji cha Park Nyigoti katika kata ya Ikoma wilayani 
Serengeti mkoani Mara baada ya kutuhumiwa kuwakamata na kuwafunga 
vitambaa usoni watu wanane wanaowatuhumu kwa uchawi  kisha kuwachapa 
viboko na kusababisha vifo vya watu watano. 
Kaimu 
kamanda wa polisi mkoa wa Mara, Kamishina msaidizi  wa jeshi la polisi 
ACP Ernest Kimola, amesema katika tukio hilo  limesababisha  watu  
wengine  watatu kujeruhiwa na viboko hivyo na kulazwa katika hospitali 
teule ya Nyerere DDH Mjini Mugumu wilayani Serengeti.
JK AKUTANA VIONGOZI WA CHAMA CHA ALBINO NCHHINI
Viongozi wa Chama Cha Albino Tanzania wakiwasili Ikulu jijini Dar es 
salaam leo Alhamisi Machi 5, 2015 kuonana na Rais Jakaya Mrisho Kikwete 
aliyewakaribisha ili kuwasikiliaza matatizo yao na kujadiliana nao 
mikakati ya namna ya kukomesha ukatili na mauaji ya watu wenye ulemavu 
wa ngozi nchini
Rais Kikwete akisalimiana na Viongozi wa Chama Cha Albino Tanzania 
Ikulu jijini Dar es salaam leo Alhamisi Machi 5, 2015 alipowakaribisha 
ili kusikiliza matatizo yao na kujadiliana nao mikakati ya namna ya 
kukomesha ukatili na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini
BAKOZI WA MAREKANI ACHOMWA VISU KOREA
BALOZI WA MAREKANI KWA KUCHOMWA KISU
Balozi wa
 Marekani nchini Korea Kusini ameshambuliwa kwa kisu usoni na pia katika
 kifundo cha mkono wake na mshambuliaji aliyekuwa akibwata kuhusiana na 
suala la kugawanywa kwa kipande cha ardhi ya serikali yao.
Mara tu 
baada ya shambulio hilo Rais wa Marekani Barack Obama amemtakia uponaji 
wa haraka msaidizi wake huyo wa zamani Mark Lippert akimuombea uponaji wa 
haraka baada tu ya shambulio lililofanywa wakati wa hotuba ya asubuhi.

Balozi 
huyo mwenye umri wa miaka 42 alikimbizwa hospitalini ambako alifanyiwa 
upasuaji wa zaidi ya saa mbili ingawa madaktari wamethibitisha majeraha 
yake hayatarishi maisha yake.
Jeraha 
lake limekadiriwa kuwa na sentimeta kumi na moja upande wa kushoto na 
ameshonwa nyuzi themanini kwenye mkono uliokatwa katika shambulio 
lililosababisha baadhi ya mishipa kushindwa kufanya kazi. Msemaji wa 
Ikulu ya Marekani amelaani kitendo hicho kwa nguvu zote. 
Baada ya 
shambulio hilo maofisa wa polisi walionekana wakimrukia na kumdhibiti 
mshambuliaji aliyekuwa na kisu chenye urefu wa inchi kumi.
Polisi 
wamemtambua mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 55 aitwaye Kim 
Ki-Jong, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya shambulio kama hilo kwa 
kumshambulia balozi wa Japan mjini Seoul mnamo mwaka 2010.
Mkuu wa 
polisi Yoon Myung na amesema kwamba wanamshikilia mtuhumiwa huyo na 
wanachunguza sababu ya shambulio hilo na masuala mengine kumhusu . Askari wakiwa wamemzunguka Balozi aliyejeruhiwa
Askari wakiwa wamemzunguka Balozi aliyejeruhiwa
Naye 
msemaji wa baraza la maridhiano na ushirikiano ambaye alikuwa ndiye 
muandaaji wa mkutano huo, ameomba radhi kwa kutokuwa na ulinzi madhubuti
 .
Balozi 
Lippert, ni mshauri wa muda mrefu wa Raisi Obama na ambaye pia aliwahi 
kuwa msaidizi wa katibu mkuu wa ulinzi katika masuala ya mahusiano na 
bara la Asia, na alipata nafasi ya kuwa balozi Korea Kusini mwezi October
 mwaka wa jana.
Lippert 
amewahi pia kushika wadhifa wa afisa wa usalama wa taifa katika 
operesheni maalum na alitwaa medali ya nyota ya shaba nyeusi wakati 
alipoitembelea Iraq.
Korea 
Kusini na Kaskazini walitengana tangu mwaka 1950-53 baada ya vita vya 
Korea na bado kiufundi wako vitani kwa kuwa mapigano yalisitishwa kwa 
suluhu .
Marekani 
na Korea Kusini wameunganisha nguvu za kijeshi na wiki hii wako katika 
mazoezi kufuatia hali tata ya kiusalama kutoka kwa wakomunisti walioko 
Kaskazini .
Pyongyang
 wanadai kuwa wanafanya mazoezi kwa kujiweka tayari na uvamizi wowote 
utakaotokea. Wakati huo huo Korea Kusini na Marekani wanadai kuwa 
mazoezi yao ni kwa kujihami tu .
Marekani inakadiriwa kuwa na vikosi vya askari wake wapatao 30,000 vya kudumu vilivyopiga katika kambi za Korea Kusini.
CHANZO BBC
Jumanne, 3 Machi 2015
JENERALI HAFTAR KAMADA MKUU WA JESHI LIBYA
        
        Viongozi wa Tobrouk, ambao wanatambuliwa na jumuiya ya 
kimataifa, wamemteua Jumatatu wiki hii Jenerali Haftar kuwa kamanda 
mkuu wa jeshi lao. Uteuzi huu umeweka matatani hali inayojiri wakati huu
 nchini Libya.
      
      Viongozi wa Tobrouk, ambao wanatambuliwa na jumuiya ya 
kimataifa, wamemteuwa Jumatatu wiki hii jenerali Haftar kuwa kamanda 
mkuu wa jeshi lao. Uteuzi huu umeweka matatani hali inayojiri wakati huu
 nchini Libya.
Khalifa Haftar amekua kiongozi wa majeshi ya serikali ya Tobrouk tangu mwaka mmoja uliyopita. Jenerali Khalifa Haftar ndiye alianzisha mashambulizi dhidi ya wanamgambo wa makundi ya kiislamu katika mji wa Benghazi.
Jenerali Khalifa Haftar alihudumu katika jeshi wakati wa utawala wa rais wa zamani wa Libya Moammar Kadhafi
Jumuiya ya kimataifa haijawahi kumhukumu wala kumuunga mkono hadharani jenerali Haftar nchini Libya.
Mwezi Mei, wakati Jenerali huyu alipoanzisha operesheni aliyoiita “Operesheni ya kiutu”, akimaanisha “ kutokomeza ugaidi”, Marekani iliona kuwa ni shambulio dhidi ya makundi hasimu yenye lengo moja. Baada ya mamia ya watu kuuawa na eneo moja la Benghazi kutekwa, mapigano yameendelea kushuhudiwa hadi leo.
Kundi la Ansar Al Shariah, lenye mafungamano na Al Qaeda, ambalo liliwekwa kwenye orodha ya makundi ya kigaidi ni moja ya makundi yanayopigana katika mji wa Benghazi na maeneo mengine nchini Libya.
Kundi hilo lilihusika pia katika shambulio dhidi ya ubalozi mdogo wa Marekani Septemba 11 mwaka 2012 na kuhusika pia katika kifo cha balozi Chris Stevens.
    
Khalifa Haftar amekua kiongozi wa majeshi ya serikali ya Tobrouk tangu mwaka mmoja uliyopita. Jenerali Khalifa Haftar ndiye alianzisha mashambulizi dhidi ya wanamgambo wa makundi ya kiislamu katika mji wa Benghazi.
Jenerali Khalifa Haftar alihudumu katika jeshi wakati wa utawala wa rais wa zamani wa Libya Moammar Kadhafi
Jumuiya ya kimataifa haijawahi kumhukumu wala kumuunga mkono hadharani jenerali Haftar nchini Libya.
Mwezi Mei, wakati Jenerali huyu alipoanzisha operesheni aliyoiita “Operesheni ya kiutu”, akimaanisha “ kutokomeza ugaidi”, Marekani iliona kuwa ni shambulio dhidi ya makundi hasimu yenye lengo moja. Baada ya mamia ya watu kuuawa na eneo moja la Benghazi kutekwa, mapigano yameendelea kushuhudiwa hadi leo.
Kundi la Ansar Al Shariah, lenye mafungamano na Al Qaeda, ambalo liliwekwa kwenye orodha ya makundi ya kigaidi ni moja ya makundi yanayopigana katika mji wa Benghazi na maeneo mengine nchini Libya.
Kundi hilo lilihusika pia katika shambulio dhidi ya ubalozi mdogo wa Marekani Septemba 11 mwaka 2012 na kuhusika pia katika kifo cha balozi Chris Stevens.
LESOTHO KUUNDA SERIKALI YA SHIRIKISHO?
Lesotho yajiandaa kuunda serikali ya muungano
Waziri
 mkuu wa Lesotho, Thomas Thabane, akipokelewa na wafuasi wake, katika 
mji mkuu wa 
Lesotho inaelekea kuunda serikali ya muungano kutokana na kile kinachoonekana kuwa hakuna atakayepata ushindi wa moja kwa moja katika Uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa juma lililopita.
      Hadi sasa chama cha Waziri Mkuu Thomas Thabane cha All Basotho 
Convention kinaongoza na tayari kimepata viti 40 vya ubunge 
ikilinganishwa na chama cha Waziri Mkuu wa zamani cha Democratic 
Congress ambacho kina viti 33.
Mshindi anahitajika kupata ushindi wa viti 61 kati ya 120 ili kuweza kuunda serikali bila ya kushirikiana na chama kingine.
Wachambuzi wa siasa nchini humo wanasema matokeo yanaonesha wazi kuwa uwezekano ni mkubwa wa kuundwa kwa serikali ya muungano.
Waangalizi wa Uchaguzi huo wanasema, zoezi hilo limekuwa huru na haki na wananchi wa Lesotho walipiga kura kwa amani.
Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga ambaye anaongoza waangalizi wa Umoja wa Afrika licha ya kuusifu uchaguzi huo kuwa huru na haki ameonya kuwa huenda kukatokea na mvutano kati ya jeshi na polisi katika nchi hiyo ikiwa mkataba wa kutoingilia siasa hautaheshimiwa.
Matokeo ya mwisho yatafahamika kesho Jumatano katika taifa hilo la Kusini mwa Afrika ambalo lililazamika kuandaa uchaguzi huo kutokana na jaribio la kuipundua serikali mwaka jana.
    
Mshindi anahitajika kupata ushindi wa viti 61 kati ya 120 ili kuweza kuunda serikali bila ya kushirikiana na chama kingine.
Wachambuzi wa siasa nchini humo wanasema matokeo yanaonesha wazi kuwa uwezekano ni mkubwa wa kuundwa kwa serikali ya muungano.
Waangalizi wa Uchaguzi huo wanasema, zoezi hilo limekuwa huru na haki na wananchi wa Lesotho walipiga kura kwa amani.
Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga ambaye anaongoza waangalizi wa Umoja wa Afrika licha ya kuusifu uchaguzi huo kuwa huru na haki ameonya kuwa huenda kukatokea na mvutano kati ya jeshi na polisi katika nchi hiyo ikiwa mkataba wa kutoingilia siasa hautaheshimiwa.
Matokeo ya mwisho yatafahamika kesho Jumatano katika taifa hilo la Kusini mwa Afrika ambalo lililazamika kuandaa uchaguzi huo kutokana na jaribio la kuipundua serikali mwaka jana.
BOKO HARAM YASHAMBULIA VISIWA ZIWA CHAD
Nchi nne zinachangia ziwa Chad : Chad, Cameroon, Niger na Nigeria.
      Idadi ya watu waliouawa katika mashambulizi hayo bado ni ya 
muda, lakini kwa mujibu wa mashahidi katika vijiji hivyo, watu tisa kwa 
uchache waliuawa.
Wanamgambo wa Boko Haram waliingia katika vijiji hivyo wakitumia mitumbwi kwenye saa mbili usiku Jumapili Machi 1, na kuanza kushambulia kwa risasi na vilipuzi katika nyumba mbalimbali za vijiji hivyo.
Katika kisiwa cha Kui Keleha, watu wawili waliuawa, na wengine walichomwa moto ndani ya nyumba zao, na wengine tena walikufa maji wakati wakijaribu kuokoa nafsi zao, kama alivyothibitisha, El Adj Aboubacar, mbunge wa Bosso.
“ Walichoma moto watu tisa kwa wakati mmoja, na mtumbwi uliyokuwa ukiwasafirisha wanawake na watoto, ambao walikuwa wakijaribu kuokoa maisha yao ulizama ziwani. Watu wanane walifariki dunia", amesema El Adj Aboubacar.
Kwa uchache watu 19 walifariki baada ya shambulio lililoendeshwa katika vijiji vya Kui Kaleha na Toumbu Buka, visiwa ambavyo vinapatikana katika ziwa Chad kwenye mpaka na Nigeria. Eneo ambalo ni vigumu kutoa ulinzi.
Karibu na eneo hilo, kijiji cha Bosso kimekuwa kikishuhudiwa mara kwa mara mashambulizi ya hapa na pale tangu Boko Haram iliposhambulia kijiji hicho Februari 6 mwaka huu.
    
Wanamgambo wa Boko Haram waliingia katika vijiji hivyo wakitumia mitumbwi kwenye saa mbili usiku Jumapili Machi 1, na kuanza kushambulia kwa risasi na vilipuzi katika nyumba mbalimbali za vijiji hivyo.
Katika kisiwa cha Kui Keleha, watu wawili waliuawa, na wengine walichomwa moto ndani ya nyumba zao, na wengine tena walikufa maji wakati wakijaribu kuokoa nafsi zao, kama alivyothibitisha, El Adj Aboubacar, mbunge wa Bosso.
“ Walichoma moto watu tisa kwa wakati mmoja, na mtumbwi uliyokuwa ukiwasafirisha wanawake na watoto, ambao walikuwa wakijaribu kuokoa maisha yao ulizama ziwani. Watu wanane walifariki dunia", amesema El Adj Aboubacar.
Kwa uchache watu 19 walifariki baada ya shambulio lililoendeshwa katika vijiji vya Kui Kaleha na Toumbu Buka, visiwa ambavyo vinapatikana katika ziwa Chad kwenye mpaka na Nigeria. Eneo ambalo ni vigumu kutoa ulinzi.
Karibu na eneo hilo, kijiji cha Bosso kimekuwa kikishuhudiwa mara kwa mara mashambulizi ya hapa na pale tangu Boko Haram iliposhambulia kijiji hicho Februari 6 mwaka huu.
HUSSEIN RADJAB ATOROKA JELA
Prosper Niyoyankana (picha), mwanasheria wa Hussein Radjabu.
Na RFI
Kiongozi 
wa zamani wa chama tawala Cndede-Fdede nchini Burundi, Hussein Radjabu 
anasadikiwa kuwa ametoroka jela usiku wa Jumapili kuamkia Jumatatu Machi
 2 mwaka 2015. Hussein Radjabu alikua akizuiliwa jela kwa kipindi cha 
zaidi ya miaka 7, tangu mwaka 2007.
Hussein 
Radjabu alifungwa jela kwa tuhuma za kupanga njama za mapinduzi dhidi ya
 utawala wa Pierre Nkurunziza. Alihukumiwa kifungo cha miaka 13 jela.
Wadadisi wanasema kutoroka kwa Hussein Radjabu ni pigo kubwa kwa utawala wa Pierre Nkurunziza.
Hata hivyo wafuasi wengi wa kinara huyo wa zamani wa chama tawala Cndede-Fdede, wanahisi kwamba huenda ameondolewa jela na kuuawa.
KUFUATIA KUONDOLEWA MASHINDANO YA KLABU BINGWA YA AFRICA AZAM YATIMUA MAKOCHA

Kocha mkuu Omo g na msaidizi wake
Uongozi wa Azam FC unatangaza kuachana na kocha wake mkuu Joseph Omog baada ya kuwa naye kwa miezi 14. Hii inatokana na timu hiyo kufungwa mabao 3-0 na timu ya El Mireikh ya Suda na kutolewa nje ya mashindano hayo.
Omog ambaye ni raia wa Cameroon ndiye aliyeipa Azam FC ubingwa wa kwanza msimu uliopita ameondolewa pamoja na msaidizi  wake Ibrahim Shikanda kutoka Kenya.
Kwa sasa timu itakuwa chini ya George Best Nsimbe. 
Habari hizi zinategemewa kuzua mjadala mkali kwa kuwa timu ya Azam ilitolewa kwa kufaniwa fujo, visa na vurugu na mashabiki wa timu ya El Mireikh. Fujo hizo ni pamoja na risasi za moto kupigwa na basi lao kupigwa mawe.
WAZIRI MKUU: SERIKALI ITATUMIA BN 55 KWA UMEME MBEYA
WAZIRI
 MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali itatumia shilingi bilioni 55 
kuvipatia umeme vijiji 244 vya mkoa wa Mbeya kupitia Miradi ya Umeme 
Vijijini (REA).
Ametoa
 kauli hiyo jana (Jumatatu, Machi 2, 2015) wakati akizungumza na 
viongozi mbalimbali wa mkoa wa Mbeya waliofika kusikiliza majumuisho ya 
ziara yake ya siku saba kwenye mkoa huo. Mkutano huo ulifanyika kwenye 
ukumbi wa Mkapa, jijini Mbeya.
“Nimeambiwa
 kuwa katika mwaka 2014/15, jumla ya vijiji 244 vitapatiwa umeme kupitia
 REA. Vijiji hivyo ni kama ifuatavyo: Chunya viko 13, Mbeya ni 32, 
Mbarali (56), Mbozi (14), Momba (15), Kyela (30), Ileje (18) na Rungwe 
(66) na jumla ya shilingi bilioni 55/- zitatumika kwa madhumuni hayo,” 
alisema.
Waziri
 Mkuu alitumia fursa hiyo kuwapongeza viongozi wa mkoa huo kwa kusimamia
 suala la usambazaji wa umeme vijijini na kukamilisha awamu ya kwanza ya
 miradi ya umeme vijijini katika vijiji 17 vya mkoa huo.
“Nimeelezwa
 kuwa miradi hiyo iliyogharamu ya shilingi billioni 7.6 katika vijiji 17
 imekamilika kwa asilimia 100. Katika  Halmashauri ya Mbeya kuna vijiji 
vitano, Mbozi vijiji vinne, Chunya vijiji sita na Rungwe vijiji viwili; 
na imeweza kuunganisha wateja 650,” alisema.
Alisema
 taarifa zinaonesha kuwa vijiji vilivyopangwa kupata umeme wa REA mwaka 
2015/2016 ni 51 na kwamba hivi sasa ujenzi wa njia kubwa ya umeme wa 
11Kv na 33Kv unaendelea. “Pia ujenzi wa njia ndogo ya umeme 400v 
unaendelea kujengwa na utekelezaji wa miradi hiyo umefikia asilimia 
42.3,” aliongeza.
Aliwahimiza viongozi wa mkoa huo kuongeza jitihada za kusambaza umeme kwa kuwa mahitaji ya umeme ni makubwa kwa wananchi wengi
RAIS AMLILIA KEPTEN KOMBA
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika hali ya majonzi wakati wasanii walipokuwa wakiimba wimbo maalumu wa kumuaga Mbunge wa Mbinga Magharibi na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Marehemu John Komba katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Spika wa Bunge, Anne Makinda. Picha ndogo ni jeneza lililobeba mwili wa Komba. Picha na Anthony Siame.
Kilio kina ushawishi mkubwa katika majanga mbalimbali hasa pindi unapomtizama mtu anayelia ni rahisi mtu mwingine kulia kutokana na yeye kuvuta hisia katika tukio husika.
Dar es Salaam. Wimbo wa John Komba aliouimba katika msiba wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1999, jana uliibua majonzi na kusababisha viongozi mbalimbali, akiwamo Rais Jakaya Kikwete, kutoa machozi ulipoimbwa kumuaga mbunge huyo.
Wimbo huo uliobadilishwa maneno yanayohusu Mwalimu Nyerere na kuingizwa yanayomtaja mbunge huyo wa Mbinga Magharibi, mbali na Rais Kikwete ulimliza pia Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, Spika wa Bunge, Anne Makinda, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Yusuf Makamba na waombolezaji wengine.
Sehemu ya mashairi ya wimbo huo uliokwenda kwa jina la “Nani Yule” ulioimbwa na wanamuziki mbalimbali wa bendi nchini, na kuwatoa watu machozi iliimbwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.
“Kapteni Komba familia yako umeiacha na nani, chama chako umekiacha na nani, nenda baba msalimie Mwalimu, mweleze hali ya Watanzania ilivyo hivi sasa, mweleze hali ya nchi yetu ilivyo hivi sasa hasa wakati huu, msalimie Mzee Kawawa Simba wa Vita”.
Baadhi ya wanamuziki walioshiriki kuimba wimbo huo ni King Kiki, Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata, Jose Mara ambaye ni mwanamuziki wa bendi ya Mapacha Watatu na Luiza Mbutu wa African Stars.
Wakati wanamuziki hao wakiendelea kuimba wimbo huo, idadi ya watu wanaolia ilizidi kuongezeka, hasa wanafamilia ndugu na jamaa wa marehemu.
Waombolezaji walisikika wakilia huku wakisema, “Jamani alikuwa akitunga nyimbo kuwaimbia wenzake waliofariki dunia, sasa leo anaimbiwa yeye.”
Alipofariki Mwalimu Nyerere Oktoba 14, mwaka 1999, aliyekuwa Mbunge wa Mbinga Magharibi, Komba akiwa na bendi ya TOT alitunga nyimbo za maombolezo ukiwamo wa “Nani Yule’, ‘Kwaheri Mwalimu’, ambazo jana zilitumiwa na wanamuziki kumuimbia yeye, wakibadilisha baadhi ya maneno.
Mwili wa mbunge huyo (61) aliyefariki dunia Jumamosi iliyopita kwa ugonjwa wa kisukari na shinikizo la damu, uliagwa katika viwanja vya Karimjee ambapo salamu mbalimbali za rambirambi zilitolewa kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda Songea mkoani Ruvuma.
Hata wakati wa kuagwa mwili huo, idadi kubwa ya wabunge wenzake waliohudhuria walishindwa kujizuia kulia huku wakikumbushana ucheshi aliokuwa nao Komba enzi za uhai wake.
Pengine msiba huo utakuwa umewagusa wengi wanaomfahamu kwa mambo mengi, na kwa kuwa kipindi hiki nchi inajiandaa kupata rais mpya, kwa kuwa kazi yake kubwa ilikuwa ni kuipigia debe CCM kupitia uimbaji wake.
Kulingana na maelezo ya waombolezaji, Mwanajeshi huyo aliyestaafu akiwa na cheo cha kapteni alikuwa ni mtu ambaye hakusita kueleza kile alichokiamini, jasiri asiyekubali kushindwa, mcheshi wakati fulani na mtu wa kutoa misaada.
Kijana mmoja ambaye alishindwa hata kutaja jina lake kutokana na kulia kwa uchungu, alilazimika kuondolewa katika viwanja hivyo baada ya kutaka kwenda kuaga tena mwili wa mbunge huyo, huku akisisitiza kuwa ndiyo aliyekuwa akimsomesha.
“Kapteni jamani umeondoka, hivi nani atanisomesha mimi. Niacheni nikamuage kwa mara nyingine huyu ni kama baba yangu mzazi, nitakuwa mgeni wa nani,” alisema kijana huyo na kuzidisha vilio, hasa kwa watoto wa marehemu.
Watu kutoka maeneo mbalimbali walifika katika viwanja vya Karimjee kumuaga mbunge huyo kuanzia saa tatu asubuhi, akiwamo mama mmoja aliyedai kuwa ametoka mkoani Mwanza kuja kuuaga mwili wa mbunge huyo.
Huku akilia mama huyo alisema, “Komba baba nimetoka Mwanza kwa ajili yako jamani, nenda ndugu yangu, nenda tu ipo siku tutaonana.”
Shughuli hiyo ilianza saa 3 asubuhi kwa wanamuziki mbalimbali wa bendi, muziki wa kizazi kipya na waigizaji wa filamu kuimba nyimbo za kumkumbuka mbunge huyo.
Wakazi wa Dar es Salaam walimiminika katika viwanja hivyo na tofauti na shughuli nyingine kama hizo, hakukuwa na ulinzi mkali wala watu kukaguliwa na vifaa maalumu.
Mara baada ya viongozi wa Serikali kumaliza kuaga mwili wa mbunge huyo, wananchi wengine nao walipewa fursa ya kuaga na kusababisha askari wa Bunge kutumia nguvu ya ziada kuwazuia kutokana na kutofuata utaratibu uliowekwa.
Watu hao walionekana kuwa na shauku ya kuaga mwili wa mbunge huyo, baadhi wakilalamikia kitendo cha kuzuiwa na askari hao wakisema kuwa Komba alikuwa mtu wa watu na wao wana haki ya kumuaga.
Hata hivyo, baadaye askari hao waliwahimiza watu hao kufuata utaratibu uliokuwa umepangwa na wote wakapata fursa ya kuaga mwili huo hadi shughuli zilipomalizika saa 7:30 mchana.
Salamu za CCM
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alisema, “Sauti ya Komba imezimika lakini imefuatiwa na sauti ya vilio vya watu waliompenda wakiomboleza. Alikuwa mwalimu, mwanajeshi, kiongozi, mbunge, mwanasiasa na mwanamuziki mwenye kipaji cha kutunga nyimbo zinazoendana na wakati.”
Kinana alisema nyimbo zilizotungwa na Komba zilitumika kuwapa hamasa wanajeshi wa Tanzania waliopigana vita vya Tanzania na Uganda mwaka 1978 hadi 1979 vilivyouondoa utawala wa Iddi Amin nchini humo.
“Katika msiba wa Mwalimu Nyerere nyimbo alizozitunga ziliwaliza Watanzania, atabaki kuwa mfano wa kuigwa. Kifo chake ni pigo wa CCM, bendi yake, wasanii na wana familia yake,” alisema Kinana na kufafanua kuwa chama hicho kimetoa rambirambi ya Sh5 milioni.
Kambi ya Upinzani
Akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Kambi ya Upinzani Bungeni, Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari alisema kifo cha Komba kimewagusa wabunge wote bila kujali itikadi zao za vyama.
“Kifo hiki kinatukumbusha kuwa hapa duniani binadamu tunapita tu. Tunatakiwa kutenda mema kwa ndugu, rafiki na Taifa letu,” alisema.
Kamati ya Bunge
Mbunge wa Mchinga na Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii ambayo Komba alikuwa makamu wake, Said Matanda alisema kuwa alizungumza na marehemu saa tano kabla ya kufikwa na mauti.
“Tulikuwa tukizungumzia safari ya kamati yetu kwenda Ethiopia ambayo ilikuwa tuifanye kesho yake (Jumapili iliyopita), lakini saa tano baadaye nikapata ujumbe kuwa amefariki dunia, sikuamini,” alisema.
Alisema marehemu alikuwa zaidi ya kiongozi kwa kutunga nyimbo zenye ujumbe mzuri kwa jamii na alikuwa na uzoefu wa miaka tisa katika kamati hiyo na ndiyo maana wajumbe wa kamati hiyo hawakusita kumchagua kuwa makamu mwenyekiti wao.
Salamu za Serikali
Akitoa salamu za Serikali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu wa Bunge), Jenista Mhagama alimwelezea Komba kama kiongozi aliyejitolea katika kila jambo.
“Juhudi na mipango aliyoifanya Komba katika jimbo lake Serikali kupitia ilani ya CCM itatekeleza. Serikali itatoa rambirambi zake kwa familia ya Komba wakati mwafaka,” alisema.
Ujumbe wa Makinda
Spika Makinda aliwataka Watanzania kuwa na tabia ya kusamehe hata kama wametendewa mambo yanayowakwaza.
“Hapa duniani tunapita tu, hatutakiwi kuwatendea watu mambo ambayo sisi hatupendi kutendewa. Tusidhani kuwa kila tunachokitaka na kukiamini kitadumu, si hivyo. Komba ameondoka kama moto wa kibatali unavyozimika,” alisema.
Makinda alisema kama Komba angepewa dakika 15 za mwisho kabla ya kufariki ili aseme jambo lolote, ni wazi kuwa angesema kama kuna aliowakosea wamsamehe.
Alisema binadamu wote ni ndugu na hata wakifa inaelezwa na viongozi wa dini kuwa wanakwenda kukutana na raha au shida ambazo zinategemea na matendo yao waliyokuwa wakiyafanya duniani.
“Wanachama wa CCM tunamwombea marehemu na tunaamini kuwa Mungu atatupa Komba mwingine,” alisema.
Salamu za familia
Msemaji wa familia ya Komba, Dominick Mwakangale alisema mwili wa mbunge huyo ambao baadaye jana jioni uliagwa na wakazi wa Songea, utazikwa leo kijijini kwake Lituhi wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.
Baadhi ya viongozi waliohudhuria ni Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara, Philip Mangula na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa.
Wengine ni Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) Jaji Damian Lubuva, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Hussein Katanga, Katibu wa Shughuli za Bunge John Joel, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Adam Kimbisa. MWANANCHI
NETANYAHU KUHUTUBIA BUNGE LA MAREKANI LEO
Obama na Netanyahu watofautiana kuhusu mpango wa kinyuklia wa Iran
Rais wa Marekani Barack Obama na Waziri mkuu wa Israel Benjamin 
Netanyahu wana mitazamao tofauti kuhusu mpango wa kinyuklia wa Iran huku
 Obama akionya kuwa Netanyahu amekuwa na mtazamo potovu kuhusu mpango 
huo
Hii leo waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu atalihutubia bunge la 
Marekani ambapo anatarajiwa kuendelea na msimamo wake kuwa mpango wa 
kinyuklia wa Iran ni kitisho kikubwa kwa Israel na una shahidi wa 
kutosha kuthibitisha hilo.Lakini Rais Obama na maafisa wake wa masuala ya sera za kigeni hawajamuachia uwanja Netanyahu kuuponda mpango wa kinyuklia wa Iran na mazungumzo yanayoendelea kati ya Iran na nchi tano zenye nguvu zaidi duniani pamoja Ujerumani, kwa kusema mazungumzo hayo ya kulenga makubaliano ndiyo njia bora zaidi ya kuusuluhisha mzozo huo.
WATATU WANUSURIKA KIFO WAKIENDA KWENYE MAZIKO YA KEPTENI KOMBA
 
 Watu zaidi ya watatu wamenusurika kifo baada ya gari yao kupata ajali eneo la Lutukila mkoani Ruvuma katika barabara kuu ya Njombe -Songea wakielekea kumzika mbunge wa Mbinga Magharibi Kepten John Komba.
Ajali hiyo ilitokea Majira ya saa 7 usiku lakini katika tukio hilo hakuna aliyepoteza Maisha zaidi ya gari kuharibika vibaya likiwa na abria watatu, wawili kati yao ni wanawake na mwanaume ni mmoja.
Wakili wa Katiba auawa Msumbiji
Mmoja wa wanaharakati wakuu wa kupigania haki za kikatiba nchini Msumbiji ameuawa kwa kupigwa risasi katika mji mkuu wa  Maputo.
Gilles
 Cistac, ambaye anaasili ya Ufaransa amehusika pakubwa katika mchakato 
wa kugawanya madaraka katika serikali ya majimbo na ugavi wa mamlaka 
nchini Msumbiji.Cistac alikuwa anapigania sera hiyo iingizwe katika katiba ya taifa jambo ambalo lilimfanya kutizamwa kama mtu anayependelea chama cha upinzani Renamo.
Afisa mkuu wa Afya katika hospitali kuu ya Maputo Joao Fumane amesema Cistac alipoteza maisha yake muda mchache baada ya kufanyiwa upasuaji.
'Mtu maarufu'
Awali msemaji wa rais Filipe Nyusi alikashifu mauaji hayo akisema kuwa hiyo ilikuwa tukio la kukera zaidi.
Mwanaharakati huyo ambaye pia ni mkufunzi katika chuo kikuu kitivo cha sheria alichangia kwa kina mchakato wa kubadilisha vipengele vya mamlaka ya urais.
Cistac alikuwa amepata uraia wa taifa hilo baada ya kuishi huko kwa tangu mwaka wa 1993.
Aidha mbali na kufundisha katika chuo kikuu cha Eduardo Mondlane, alikuwa amehudumu kwa kipindi kirefu kama mshauri wa maswala ya sheria katika wizara mbalimbali.
Katika miaka ya hivi punde kulikuwa na shauku ya kuzuka upya vita vya wenyewe kwa wenyewe baada ya kundi la Renamo, kulalamika kuwa uchaguzi uliofanywa nchini humo haukuwa wa haki.
Renamo ilisitisha mapigano mwaka wa 1992 baada ya kukabiliana na serikali kwa kipindi cha miaka 16.
Kiongozi wake Afonso Dhlakama alikubalia mwito wa kujaribu kutafuta uwiano kupitia kwa bunge la taifa.
Inaaminika kuwa rais Filipe Nyusi, ndiye aliyewashawishi wabunge wa Renamo kujiunga na serikali .
Chama hicho kilichojizolea asilimia 36% ya kura za urais zilizopigwa mwezi Oktoba.
Mpinzani wa Urusi aliyeuwawa azikwa
Waombolezaji nchini Urusi wamejitokeza nje ya kituo cha haki za binadamu
 mjini Moscwo kwa ajili ya kuhudhuria maziko ya kiongozi wa upinzani 
aliyeuwawa Boris Nemtsov.
Kiongozi huyo wa upinzani aliuwawa kwa kupigwa risasi ijumaa jioni 
wakati akitembea kwenye daraja la karibu na ikulu ya Kremlin akiwa 
pamoja na mpenzi wake. Hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na 
tukio hilo.Mwili wa marehemu Nemtov umelazwa kwenye sanduku ukiwa umevishwa sanda nyeupe katika kituo cha haki za binadamu cha Sakharov mjini Moscow, kituo ambacho kimepewa jina la aliyekuwa mpinzani enzi za utawala wa kisovieti na aliyewahisi kutunukiwa tuzo ya amani ya Nobel Andrei Sakharov. Mauaji ya kiongozi wa upinzani wa Urusi Boris Nemtsov yameitikisa kwa kiasi kikubwa jamii ya vuguvugu dogo öla upinzani na ambalo limetengwa nchini Urusi.
Wengi wa wafuasi wa upinzani nchini humo wanashuku mauaji hayo yamefanywa kwa amri ya serikali ya Urusi kama hatua ya kulipiza kisasi kauli za mpinzani huyo za kumkosoa rais Vladmir Putin. Maafisa wa Urusi wameashiria kwamba kuna uwezekano mkubwa wa sababu zamauaji hayo kuwa zimetoakana pia na uchokozi ulioonekana kulenga kumchafua rais Putin. Nemtsov anazikwa leo mjini Moscow wakati ambapo baadhi ya wabunge maarufu kutoka Ulaya wamearifu kwamba wamezuiwa na nchi hiyo ya Urusi kuhudhuria maziko hayo.
Mabalozi wengi wa nchi za magharibi walitarajiwa kuhudhuria shughuli ya maziko iliyoanza asubuhi ya leo kwenye kituo cha Sakharov kabla ya maiti kuzikwa mchana wa leo kwenye makaburi yaliyoko nje ya eneo hilo. Hadi sasa kuna wawili mashuhuri kutoka Ulaya waliosema wamezuiwa na Urusi kuhudhuria maziko hayo.
Aliyekuwa waziri wa nje wa Latvia Sandra Kalniete ambaye ni mbunge katika bunge la ulaya amesema lizuiwa na walinzi kuingia kwenye uwanja wa ndege wa Sheremetyevo mjini Moscow jana usiku.Mbunge huyo ametoa taarifa baada ya kuzuiwa uwanja wa ndege akisema licha ya uamuzi huo wa serikali ya Putin anataka kuifahamisha familia ya Nemtsov pamoja na marafiki zake na wananchi wote wa Urusi wanaounga mkono Demokrasia watambue kwamba Ulaya ipo pamoja nao wakati huu wa majonzi.
Mwingine aliyezuiliwa na Urusi kuhudhuria maziko hayo ni rais wa baraza la seneti la Poland Bogdan Borusewicz aliyesema kwamba amenyimwa visa ya kuingia nchini humo.Shahidi mkuu wa tukio la mauaji ya Nemtsov ni mpenzi wake aliyekuwa naye wakati huo wa tukio Anna Duritsskaya ambaye anaendelea kushirikiana na kamati ya uchnguzi.Hata hivyo bibi huyo amerudi nyumbani kwao Ukraine.
Mwandishi:Saumu Mwasimba
LEO NI SIKU YA WANYAMAPORI NA MAZAOPORI:BAN KI MOON AIONYA DUNIA
Leo
 ni siku ya wanyama na mazao ya porini duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa 
Mataifa Ban Ki-moon ametaka umakini zaidi katika kushughulikia vitendo 
vya uhalifu dhidi ya maliasili hiyo.
Katika ujumbe wake, Ban 
amesema biashara haramu ya wanyamapori na bidhaa zitokanazo na viumbe 
hivyo ikiwemo ndovu, magogo na faru, imekuwa ikiibuka na mbinu mpya 
kila uchao na hata kuzidi ile ya usafirishaji haramu wa binadamu na dawa
 za kulevya.Amesema kushamiri huko kunapigiwa chepuo na rushwa na uongozi dhaifu akiongeza kuwa kuna ushahidi thabiti wa kuhusika kwa mitandao ya kihalifu iliyopangwa na vikundi vilivyojihami.
Ban amesema biashara hiyo haramu siyo tu inakwamisha utawala wa sheria bali pia unatishia usalama wa taifa na ni kikwazo kikubwa kwa juhudi za wanavijiji na jamii za watu wa asili za matumizi endelevu za maliasili.
Kwa mantiki hiyo Katibu Mkuu ametaka umakini wa kushughulikia uhalifu huo akitaka ushiriki wa jamii zote zinazohusika na matumizi ya maliasili hizo kwa ajili ya dawa, chakula, ujenzi, samani, urembo na nguo.
Amesema endapo usimamizi wa sheria utakwenda sambamba na ushirikishi wa jamii nzima kutawezesha kumaliza tatizo la matumizi haramu ya bidhaa za porini
ANGALIA MELI KUBWA LAO
Siku chache zilizopita, meli kubwa kuliko zote duniani iliwasili 
nchini Uingereza na kuwa kivutio kikubwa.Meli hiyo ya mizigo ina uwezo 
wa kubeba makontena 19,100 na ukubwa wake ni sawa na viwanja vinne vya 
kuchezea mpira.
Meli hiyo imesajiliwa Hong Kong na ilitentengenezwa nchini China, ina
 uwezo wa kubeba tani 57,000 ambao ni uzito mkubwa zaidi unaoweza 
kuchukuliwa na chombo cha usafiri duniani.
Ilisafiri kwa mwezi mzima kutoka Shanghai China hadi nchini Uingereza.
HOTUBA YA MHE JK YA MWEZI WA PILI HII HAPA
Jumatatu, 2 Machi 2015
JK AONGOZA MAMIA KUMWAGA HAYATI KEPTEN JOHN KOMBA
Rais Kikwete (katikati) akiwa na makamu wake Gharib Bilal
(kushoto) na Anna Makinda katika viwanja vya Karimjee ili kumuaga marehemu
Kapteni John Komba.
Rais Mstaafu Benjamin Mkapa (wa pili kulia) akiwa na mkewe
Anna (wa tatu kulia) wakiwasili viwanja vya Karimjee.
Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa (kulia) akisalimiana
na Mkapa.
Jumapili, 1 Machi 2015
NDEGE YA JESHI YAANGUKA MWANZA
Muonekano wa ndege ya ndege ya jeshi baada ya kuanguka leo uwanja wa ndege wa Mwanza.(Picha na Mtandao)
NDEGE ya kijeshi imeanguka tarehe 27/2/2015 uwanja wa ndege wa Mwanza na 
kusambaratika  wakati inatoka kaskazini mwa uwanja huo kuelekea kusini 
ambapo rubani wake, Peter Augustino Lyamunda, amevunjika mguu.
Chanzo cha ajali hiyo ni ndege aliyeingia kwenye moja ya  
injini za ndege hiyo ilipotaka kuruka,  ikashindwa na kuanguka.
Ndege wanaozurura kwenye uwanja huo wamekuwa ni tatizo na wameripotiwa kulalamikiwa na marubani. Hata hivyo kuwaua ndege hao kunaweza kuaua malalamiko kwa watetezi wa haki za wanyama. 
Jisajili kwenye:
Maoni (Atom)
 







