Na Berdina Majinge
Basi hilo, lifanyalo safari zake kati ya Iringa na
Njombe, lilipata ajali hiyo saa 1:45 usiku wa kuamkia jana wakati dereva
alipokuwa akijaribu kuyapita magari mengine kabla ya kugongana uso kwa
uso na lori.
Watu 23 wamekufa papo
hapo na wengine 34 kujeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya Another G
kugongana na lori eneo la Kinyanambo A, Mafinga wilayani Mufindi, ikiwa
ni takriban miezi mitatu baada ya ajali nyingine iliyoua watu 50 katika
wilaya hiyo.
Basi hilo, lifanyalo safari zake kati ya Iringa na
Njombe, lilipata ajali hiyo saa 1:45 usiku wa kuamkia jana wakati
dereva alipokuwa akijaribu kuyapita magari mengine kabla ya kugongana
uso kwa uso na lori.
Kaimu kamanda wa polisi wa Mkoa wa Iringa,
Pudenciana Protas alisema basi hilo lilikuwa likiendeshwa na Nicholaus
Mangula (29) na lori la Kampuni ya Bravo Logistics lililokuwa
likiendeshwa na Rogers Mdoe (39) na ambalo lililikuwa likitokea Zambia
kuelekea Dar es Salaam.
Katika ajali hiyo, dereva wa lori alifariki dunia papo hapo.
Machi 10 mwaka huu, watu 50 walipoteza maisha
kwenye ajali iliyotokea Mafinga, Changarawe, wakati kontena lililokuwa
limebwa na lori lilipochomoka wakati dereva akijaribu kukwepa mashimo
barabarani na kuangukia kwenye lori.
Alisema majeruhi wamelazwa Hospitali ya Wilaya ya
Mufindi mjini Mafinga na maiti zimehifadhiwa hospitalini hapo ikiwamo ya
dereva wa lori aliyekufa papo hapo.
Alisema chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa
basi la Kampuni ya Another G ambaye alikuwa kwenye mwendo kasi na
alikuwa akiyapita magari mengine bila tahadhari ndipo alipofika katikati
alikutana na lori na kuamua kulichepusha nje ya barabara hali
iliyosababisha kupinduka na kisha lori kuligonga basi hilo ubavuni.
Alisema baada ya ajali hiyo, dereva wa basi alikimbia lakini polisi wamemkamata na yupo chini ya ulinzi.
Waliokufa na kutambuliwa mpaka sasa ni Lukas
Pascal, Brasto Samila, Dickson Luvanda, Albert Silla, Rogers Mdoe, Eva
Mbalinga, Hadija Mkoi, Clemence Mtati, Mohamed Kalika, Kastoli
Mwakyamba, Damian Myala na Sillo Nziku.
Waliojeruhiwa ni Majoline Lupembe (23) mkazi wa
Iringa, Veronica Simba (20, Tabora), Shadia Ally (24, Iringa), Mariam
Mbise (23, Mafinga), Anita Makwela (24, Kilolo), Benita Sagala (18,
Njombe), Bertha Mkoi (27), Rahel Mavika (18, Mufindi), Selina Fulgence
(23, Kigoma) na Maria Mwenda (17) mkazi wa Mafinga.
Majeruhi wengine ni Ndipako Mbilinyi (23, Njombe),
Alexander Mkakazii (28, Mafinga), Meshack Kibiki (44, Mafinga), Simon
Jumbe (22, Singida), Jerry Lutego (36, mkazi wa Mafinga), Enock Kanyika
(18, Mafinga), Deogratius Kayombo (21, Mafinga) na Yusuph Lulanda (22)
mkazi wa Njombe.
Wengine waliojeruhiwa ni Petro Mwalongo (21,
Njombe), Paulo Chane (21, Kilolo), Kenned Msemwa (28, Njombe), Mode
Shiraz (21, Singida), Emmanuel Antony (21, Mwanza), Godfrey Kanyika (39,
Mafinga) na Boniface Bosha (20).